Facebook

Saturday 28 June 2014

Moyes mbioni kujiunga Galatasaray.


Aliyekuwa kocha wa Manchester United David Moyes ameahidiwa kitita cha pauni milioni £4 kwa mwaka ilikumrithi Roberto Mancini kama kocha wa Galatasaray ya Uturuki.
Iwapo mkataba huo utakubalika na ''The Chosen one '' huenda raiya huyo wa Scotland akarejea katika safu ya ukufunzi miezi michache tangu atimuliwe huko Old Trafford kufuatia msururu wa matokeo duni.
Kibarua chake kiliota nyasi huko Old Trafford mwezi aprili Manchester ikiwa katika nafasi ya saba katika ligi ya Uingereza msimu mmoja tu tangu watwae ubingwa chini ya mkufunzi shupavu Sir alex fergusson.
Galatasaray imedhibitishia waandishi wa habari kuwa Moyes alizuru Istanbul ilikufanya mkutano na rais wa klabu hiyo Unal Aysal.

Hata hivyo klabu hiyo iliweka wazi niya yao ya kuwasajili but described Mjerumani Joachim Low ama Jurgen Klinsmann .
Galatasaray, ilimaliza katika nafasi ya pili msimu iliokwisha nyuma ya Fenerbahce japo mabingwa hao wamepigwa marufuku ya kushiriki ligi ya mabingwa barani uropa kwa udanganyifu katika baadhiya mechi zao.
Hii haitakuwa mara ya kwanza kwa vigogo hao wa ligi ya Uturuki Kufunzwa na Muingereza ,mwaka wa 1995 waliwahi kufunzwa na kocha Graeme Souness.

0 comments:

Post a Comment