Mchezaji kinda wa Kiingereza anayekipiga klabu ya Southampton Luke Shaw,ambaye alikuwa na timu ya taifa ya Uingereza katika michuano ya kombe la dunia inayoendelea nchini Brazil ingawa timu yao ya taifa imeshindwa kufuzu hatua ya mtoano.
Kwa taarifa zilizotufikia ni kwamba ada ya uhamisho iliyotolewa na Manchester United inayokadiriwa kuwa kati ya Paundi milion 28 hadi 30 imekubaliwa na klabu yake ya Sothampton na anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya leo hii katika hospitali ya mashetani wekundu tayari kwa kujiunga na klabu hiyo.
Huku Patrice Evra akiwa ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja na Kuondoka kwa kinda mwingine aliyekuwa anacheza nafasi hiyo Alexander Buttner aliyekubali kujiunga Dyanamo Moscow mwanzoni mwa wiki hii kunatoa nafasi ya kinda huyo kujiunga na mashetani wekundu ambao tayari wameshaanza kuimarifa safu yao ya kiungo kwa kumsajili kiungo machachari kutoka Athletico Bilbao,Ander Herrera.
Akiwa maeonekana kwenye michezo 60 ya klabu ya Southampton Luke Shaw ataweka rekodi ya kinda aliyesajiliwa kwa dau la fedha kubwa zaidi duniani.Huku akiwa amemzidi kete aliyekuwa beki wa Chelsea na timu ya taifa ya Uingereza Ashley Cole na kuchukua nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa.
Luke Shaw alianza kucheza kwa mara ya kwanza katika timu yake ya Sothampton kutoka katika shule ya kukuzia vipaji ya klabu hiyo akiwa na miaka 16 mwaka 2012.
SOURCE:SKY SPORT
Imeandaliwa na.....
Katemi Methsela
Tumehamia
katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali
kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi
vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com
Related Posts:
Manchester United yamnasa ramnasa rasmi "beki kisiki"Marcos Rojo.
Manchester United imetangaza rasmi kumsaini Beki wa Sporting Lisbon,Marcos Rojo kwa ada ya Euro Milioni 20 na kumpa
Mkataba wa Miaka Mitano.Kwenye dili hiyo,Luis Nani amekwenda Sporting Lisbon kwa Mkopo wa Msimu mmoja.
HIST… Read More
Yaya Toure "Nataka kubaki Etihad"
Yaya Toure anataka kusalia Etihad kwa miaka zaidi.
Kiungo cha kati wa Ivory Coast na Manchester City ya Uingereza Yaya Toure amesema kuwa angependa kusalia Etihad milele.
Awali ripoti zilikuwa zimeashiria kutoridhis… Read More
TETESI ZA USAJILI KATIKA MAGAZETI MBALIMBALI BARANI ULAYA NA BantuTz.com
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers
amesema hana mpango wa kumchukua Mario
Balotelli kutoka AC Milan, baada ya mchezaji
huyo kuhusishwa na Anfield (Daily Mirror),
>Manchester City wanakaribia kukamilisha
usajili wa beki w… Read More
Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya.
Beki was Aston Villa Ron Vlaar, 29, atakuwa na mazungumzo na meneja
wake Paul Lambert kuhusiana na hatma yake licha ya Southampton kumwania
(Daily Mirror),
QPR wanafikiria kumchukua kiungo wa Colombia Carlos… Read More
Origi rasmi Liverpool.
Liverpool wamekamilisha usajili wa mshambuliaji wa Ubelgiji Divock
Origi kutoka Lille kwa pauni milioni 10. Origi, 19, amesaini mkataba wa
miaka mitano, lakini atasalia Ufaransa na klabu yake ya Lille kwa mkopo
kwa msimu… Read More
0 comments:
Post a Comment