Facebook

Thursday, 26 June 2014

Southampton yakubali Luke Shaw kusajiliwa Manchester United.

      Mchezaji kinda wa Kiingereza anayekipiga klabu ya Southampton Luke Shaw,ambaye alikuwa na timu ya taifa ya Uingereza katika michuano ya kombe la dunia inayoendelea nchini Brazil ingawa timu yao ya taifa imeshindwa kufuzu hatua ya mtoano.
          Kwa taarifa zilizotufikia ni kwamba ada  ya uhamisho iliyotolewa na Manchester United inayokadiriwa kuwa kati ya Paundi milion 28 hadi 30 imekubaliwa na klabu yake ya Sothampton na anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya afya leo hii katika hospitali ya mashetani wekundu tayari kwa kujiunga na klabu hiyo. 

     Huku Patrice Evra akiwa ameshasaini mkataba wa mwaka mmoja na Kuondoka kwa kinda mwingine aliyekuwa anacheza nafasi hiyo Alexander Buttner aliyekubali kujiunga Dyanamo Moscow mwanzoni mwa wiki hii kunatoa nafasi ya kinda huyo kujiunga na mashetani wekundu ambao tayari wameshaanza kuimarifa safu yao ya kiungo kwa kumsajili kiungo machachari kutoka Athletico Bilbao,Ander Herrera.

  Akiwa maeonekana kwenye michezo 60 ya klabu ya Southampton Luke Shaw ataweka rekodi ya kinda aliyesajiliwa kwa dau la fedha kubwa zaidi duniani.Huku akiwa amemzidi kete aliyekuwa beki wa Chelsea na timu ya taifa ya Uingereza Ashley Cole na kuchukua nafasi yake katika kikosi cha timu ya taifa.

     Luke Shaw alianza kucheza kwa mara ya kwanza katika timu yake ya Sothampton kutoka katika shule ya kukuzia vipaji ya klabu hiyo akiwa na miaka 16 mwaka 2012.

SOURCE:SKY SPORT

Imeandaliwa na.....
                                Katemi Methsela


Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

  • Van Gaal amafungia kazi kiungo SchweinsteigerMchezaji nyota wa Bayern Munich Bastian Schweinsteiger anabaki chaguo namba moja la timu ya Manchester United kwa nafasi ya kiungo msimu huu.Lakini United wapo tayari kumpata mchezaji kiungo wa Southampton Morgan Schneide… Read More
  • Arsenal yamtengea dau Kondogbia.Hakuna timu ambayo ipo nyuma kupata wachezaji wazuri kwa ajili ya msimu ujao. Ukikaa nyuma muda wa usajili maisha hayatakua mazuri muda wa msimu ujao. Arsenal inakomaa kumpata mchezaji Kondogbia ambae pia anatakiwa na Inter m… Read More
  • Mbeya City yazidi kubomolewa   Mara baada ya Peter Mwalyanzi pamoja na Deus Kaseke kuondoka katika timu hiyo baada ya kusajiliwa na vilabu vya Simba na Yanga leo tena wameondoka wengine. Pichani hapo ni Paul Nongwa na Anthony Matogolo leo wamej… Read More
  • Falcao akubali kutua Chelsea.Kama BantuTz tulivyo ripoti hapo mwanzoni kwamba mama yake Falcao alisema kwamba mwanae hana furaha ndani ya Manchester united. Kwa hiyo lazima alikua anatarajiwa kuondoka Old Trafford baada ya msimu kuisha. Habari ikufikie k… Read More
  • Gundogan atua Man UnitedManchester united imezipiku timu za Bayern Munich na Barcelona kwenye vita ya kupata saini ya mchezaji wa Borussia Dortmund. Mchezaji huyo ambae anacheza sehemu ya kiungo amekubaliana mambo ya msingi na Manchester united. Gun… Read More

0 comments:

Post a Comment