Facebook

Sunday 29 June 2014

Muimbaji wa Nigeria atoa bikira yake kwa Boko Haram

Mwanamuziki, muigizaji na balozi wa amani wa Umoja wa Mataifa Adokiye amesema yuko tayari kujitolea bikira yake kwa Boko Haram ili wawaachie wasichana waliowateka nyara.
  Mwanamuziki, muigizaji na balozi wa amani wa Umoja wa Mataifa Adokiye amesema yuko tayari kutoa bikira yake kwa Boko Haram ili wawaachie wasichana waliowateka nyara.
Mwimbaji wa pop wa nchini Nigeria na balozi wa amani ametuma maoni ya kushtusha kwenye mtandao wa kijamii kwa kudai anatoa bikira yake kwa wanamgambo wa Kiislamu ili wawaachie mamia ya wasichana wa shule waliowateka nyara.
        Adokiye, 23, alitoa mapendekezo hayo kwa wanachama wa Boko Haram ili waweze kuwaachia huru wasichana wa Nigera wapatao 276 ambao waliwachukua mwezi Aprili katika mji wenye Wakristo wa kaskazini-mashariki wa Chibok.
Muimbaji na muigizaji huyo anayetokea jimbo la Imo aliliambia gazeti la Nigeria la Vanguard: ‘Hii ni saa 5 usiku, unajua ninachokifikiria?, wale wasichana wadogo, wako wapi saa hii, nini kitakuwa kinatokea kwao.
Kiongozi wa kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Boko Haram Abubakar Shekau ambaye aliongoza utekaji nyara wa wanafunzi wasichana wapatao 276 nchini Nigeria.
Kiongozi wa kundi la wanamgambo wa Kiislamu la Boko Haram Abubakar Shekau ambaye aliongoza utekaji nyara wa wanafunzi wasichana wapatao 276 katika jimbo la Chibok, Nigeria.
“Sio haki . bado ni wadogo. Natamani ningejitoa mimi tubadilishane.”
Balozi huyo wa amani wa Umoja wa Mataifa aliongeza: “Kuna wenye umri kati ya miaka 12 na 15. Nimekuwa na nina uzoefu. Hata wanaume 10 mpaka 12 wanaweza kunichukua kila usiku, sijali. Hebu waachieni hao wasichana, warudi kwa wazazi wao”.
Utekaji, ulioongozwa na kiongozi wa kundi hilo Abubakar Shekau, umeibua kampeni kubwa duniani ya #BringBackOurGirls. Imekuwa ikiungwa mkono na viongozi wakubwa kama David Cameron na Michelle Obama japo watumiaji wa Twitter hawana uhakika na manufaa ya ofa ya Adokiye.



Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com
 

0 comments:

Post a Comment