Mshambuliaji wa Italia, Mario Balotelli, 24,
amekamilisha uhamisho wake kutoka AC
Milan kwenda Liverpool kwa pauni milioni
16. Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester
City, amekubali mkataba wa muda mrefu,
ingawa hatoweza kucheza dhidi ya timu yake
ya zamani Jumatatu usiku. Balotelli aliondoka
City miezi 17 iliyopita baada ya kupachika
mabao 30 katika misimu mitatu.
"Uhamisho huu unawakilisha misingi ya klabu
na nadhani tumefanya biashara nzuri tu
hapa," amesema bosi wa Liverpool, Brendan
Rodgers. Balotelli, ambaye atavaa jezi namba
45, amesema alifanya makosa kuondoka
England mwaka jana. "Nimefurahi kurejea
tena, kwa sababu nilifanya makosa kuondoka
England," amesema na kuongeza "Nilitaka
kwenda Italy, lakini nikagundua ni makosa."
Monday, 25 August 2014
BALOTELLI AJIUNGA RASMI LIVERPOOL
Related Posts:
Real Madrid yamtimua Carlo Ancelloti.RASMI: Real Madrid imevunja mkataba na kochawake Carlo Ancelotti baada ya kuinoa kwa miaka miwili.Katika msimu wake wa kwanza Bernabeu, Ancelotti alishinda ligi ya mabingwa, Copa del Rey, Uefa Super Cup na kombe la klab… Read More
YANGA YAZIDI KUJI IMARISHA,YAONGEZA WENGINE WAWILI.YANGA SC imeendelea na usajili wa wachezaji wapya kuelekea msimu ujao na leo vifaa viwili vimemwaga wino makao makuu ya klabu,Jangwani. Beki wa kushoto MwinyiHajji Mngwali amesainimiaka miwili na kipa Benedicto Tinocco kutoka… Read More
BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika magazeti yote ya leo Jumanne,Mei 26. MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata habari nuhim… Read More
SIMBA YAJIBU MAPIGO YASAJILI WAWILI:SIMBA SC imesajili mabeki wawili wa Kizanzibari, Samir Hajji Nuhu wa kushoto na Mohammed Fakhi wa kati usiku wa leo. Nuhu alikuwa mchezaji wa Azam FC kwa misimu miwili hadi msimu wa 2013/2014 kabla ya kuumia goti nakuondolewa… Read More
BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika kuarasa za magazeti yote ya leo Jumatano,Mei 27. MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata habari… Read More
0 comments:
Post a Comment