Msichana wa miaka tisa nchini Marekani
amemuua kwa kumpiga risasi, kwa bahati
mbaya, mwalimu wake aliyekuwa
akimfundisha jinsi ya kutumia bunduki.
Mwalimu huyo alikuwa akimpa mafunzo
msichana huyo katika kituo cha kupigia risasi
kilichopo Arizona, wakati msichana huyo
alipopoteza mwelekeo baada ya kufyatua
risasi ya kwanza, katika bunduki aina ya Uzi.
Mwalimu huyo, Charles Vacca, 39, alipigwa
risasi kichwani na kufariki wakati akipelekwa
hospitali kwa ndege mjini Las Vegas.
Msichana huyo alikuwa katika kituo hicho
pamoja na wazazi wake.
Ajali hiyo ilitokea Jumatatu iliyopita katika
kituo cha kupiga risasi cha Last Stop,
kilichopo White Hills, Arizona.
Waandishi wa habari wanasema ni jambo la
kawaida katika maeneo mengi nchini
Marekani kwa watoto kufunzwa jinsi ya
kutumia bunduki.
Vituo vingi vya kupigia risasi huwa vina
sheria kali za usalama hasa kwa watoto.
Haifahamiki kituo hicho kina kanuni zipi
kuhusiana na umri wa chini ambao watoto
wanaruhusiwa kuanza mafunzo.
Wednesday, 27 August 2014
Mtoto amuua Mwalimu wake kwa kumpiga risasi Marekani.
Related Posts:
Washambuliaji wauwawa magharibi Uganda Askari wa usalama wa Uganda wanasema kuwa watu kadha wameuwawa katika shambulio lilofanywa na watu waliokuwa na silaha, magharibi mwa nch… Read More
Watu 20 wauawa katika mashambulio mawili katika Pwani ya Kenya. Watu wasiopungua 20 wameuawa katika mashambulio mawili katika kaunti mbili kwenye pwani ya Kenya usiku wa kuamkia Jumapili. Watu walioshuhudia matukio hayo wamesema, watu wenye silaha nzito walishambulia eneo … Read More
Israel: Tumewakamata washukiwa wa mauaji Taarifa kutoka nchini Israeli zinasema kuwa serikali inawazuia baadhi ya watu kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya kijana wa kipalestina… Read More
Watu zaidi ya 50 wauawa Uganda. Watu wasiopungua 50 wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia vituo vya polisi na kambi za jeshi nchini Uganda, kwa mujibu wa jeshi. Miongoni mwa waliokufa ni washambuliaji 41 na polisi pamoja na raia 17… Read More
Ebola yaanza kuonekana Ghana. Ghana inatibu mtu mmoja anayedhaniwa kuwa na Ebola, kwa mujibu wa wizara ya afya. Ebola imesababisha vifo vya zaidi ya watu 460 mpaka sasa tangu ugonjwa huo ulipoanza nchini Guinea mwezi Februari, na kusam… Read More
0 comments:
Post a Comment