Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano
Ronaldo ameshinda tuzo ya mchezaji bora wa
Uefa, na kuwapiku kipa wa Bayern Munich,
Manuel Neuer na Arjen Robben.
Ronaldo, 29, kutoka Ureno alipachika mabao
17 na kuisaidia Real Madrid kunyakua Kombe
la Klabu Bingwa Ulaya - Uefa Champions
League- msimu uliopita.
"Nimefurahi sana, kwa hiyo lazima
niwashukuru wachezaji wenzangu kwa sababu
bila timu, tuzo binafsi ni vigumu kuzipata."
Amesema Ronaldo.
Ronaldo aliwazidi Neuer na Robben katika
kura zilizopigwa na jopo la waandishi wa
habari 54.
Neuer, 28, aliisaidia Ujerumani kushinda
Kombe la Dunia, huku Robben, 30, akifunga
magoli 21 ya Bayern na matatu kwa timu ya
taifa ya Uholanzi iliyofika nusu fainali Brazil.
Ronaldo alifunga mabao matatu - hat-trick -
wakati Ureno ilipoichapa Sweden katika
mchezo wa kufuzu kucheza Kombe la Dunia,
ingawa hakuweza kuwika Brazil, kwani Ureno
ilitolewa katika ngazi ya makundi.
Hata hivyo, kiwango chake katika ngazi ya
klabu kiliweza kushawishi jopo lililopiga kura,
ambalo lilitakiwa kuchagua mshindi kati ya
watatu hao baada ya mchujo kutoka
wachezaji 10.
Friday, 29 August 2014
RONALDO MCHEZAJI BORA WA UEFA
Related Posts:
Azam FC- Hatujamzuia Kavumbagu Kwenda BurundiUongozi wa Azam FC umesema haujamzuia mshambuliaji wake wa kimataifa, Didier Kavumbagu kurejea kwao kuitumikia timu yake ya taifa ‘Entamba Murugamba’.Katika taarifa yake, Msemaji wa Azam FC Jaffar Idd Maganga,ames… Read More
BantuTz MAGAZETINI:SOMA KILICHOANDIKWA KATIKA KURASA ZA MAGAZETI YOTE YA LEO APRIL 1,2014. BantuTz MAGAZETINI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikwa k… Read More
Viongozi CECAFA wamuunga Mkono BlatterRais wa Baraza la Vyama vya Soka Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Leodegar Tenga amesema Rais wa Shirikisho la Soka Ulimwenguni FIFA, Sepp Blatter amepewa nafasi na viongozi wa Soka Barani Afrika katika kushinda Uchaguzi Mk… Read More
BantuTz MAGAZETINI:SOMA KILICHOANDIKWA KATIKA KURASA ZA MAGAZETI MBALIMBALI YA LEO MACHI 31,2015. BantuTz MAGAZETINI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikwa k… Read More
CHICHARITO "REAL MADRID NI MAJANGA"Mshambuliaji Javier Hernadez " "Chicharito" amesema kuendelea kukaa benchi katika klabu ya Real Madrid kunamfanya akose furaha na kukosa kujiamini. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico alijiunga na mabingwa hao wa Ulaya mwanz… Read More
0 comments:
Post a Comment