Bwana mmoja nchini Brazil ameibuka saa mbili baada ya kutangazwa kuwa amekufa.Mtu huyo mwenye umri wa miaka 54
Valdeluco de Oliveira, ambaye alikuwa anaugua saratani alipelekwa hospitali baada ya kulalamika kusumbuliwa na matatizo ya kupumua. Kikosi cha madaktari katika jimbo la kaskazini mashariki la Bahia kiliwaambia ndugu zake kuwa bwana de Oliveira alikuwa amekufa baada ya kupata mishtuko miwili ya moyo.
Ndugu hao walisaini cheti cha kifo na kuupeleka mwili wake katika chumba cha kuhifadhi maiti. Saa mbili baadaye, wafanyakazi wa hospitali waliona mwili wa mtu ukitikisika na kwenda haraka kumsaidia.Hospitali hiyo, katika mji mkuu wa jimbo la Salvador imeanzisha uchunguzi juu ya suala hilo. Mama wa Bwana Oliveira amesema maombi yake ya maajabu kutokea,yamejibiwa.
Tuesday, 26 August 2014
Mtu aliyekufa;afufuka Brazil.
Related Posts:
BantuTz MAGAZETINI:SOMA KILICHOANDIKWA KATIKA MAGAZETI YOTE YA LEO MEI 12 BantuTz MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusoma na kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata hab… Read More
Volcano ya ajabu yalipuka Chile.Volcano aina ya Calbuco imelipuka kwa muda mfupi huko nchini Chile ikiwa ni mara ya kwanza ndani ya zaidi ya miaka 40. Watu waliokuwa wakiishi maeneo jirani na ulikotokea mlipuko wa Volcano hiyo wamelazimika kuyahama makazi y… Read More
Watu zaidi ya 5000 wafariki dunia baada ya tetemeko kubwa la ardhi huko Nepal.Idadi ya watu ambao wamethibitishwa kuaga dunia wakati kulipotokea tetemeko kubwa la ardhi nchini Nepal siku ya Jumamosi imepanda hadi zaidi ya watu 5000. Utawala unasema kuwa zaidi ya watu 10,000 walijeruhiwa. Serikali ya Ne… Read More
Jeshi la Nigeria lawaokoa watoto wa kike 293 kutoka katika kambi ya Boko Haram.Jeshi la Nigeria limesema limewaokoa watoto wa kike mia mbili na akina mama tisini na tatu kutoka katika kambi ya Boko Haram iliyoko katika msitu wa Sambisa, kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Jeshi hilo limesema watoto hao … Read More
Kanisa labadilishwa kuwa msikiti Iceland. Iceland imezua hisia kali wakati wa ufunguzi wa maonyesho ya usanii katika mji wa Venice nchini Italy baada ya kulibadilisha kanisa ambalo lilikuwa halitumiki kuwa msikiti. Kwa jina 'La Moschea' msikiti huo unat… Read More
0 comments:
Post a Comment