Umri wa Jose Mujica ni miaka 78 ambapo May 20 mwaka huu alitimiza miaka 79
1. Yani nguo zake zinafuliwa kawaida na kuanikwa nje tu, pia maji anayotumia ni ya kisima ambacho kina magugu mengi.
2. Analindwa na Polisi wawili na mbwa na aliikataa kukaa kwenye nyumba 
ya serikali aliyopewa na badala yake kaenda kuishi kwenye nyumba ya mke 
wake huko mashambani ambako kuna mazingira ya kimasikini sana ikiwemo 
barabara mbovu nje kidogo ya mji wa Montevideo.
3. Rais na mkewe hufanya kazi ya kuotesha maua wao wenyewe yakiwa ni maisha ya kipekee kusikia ni ya Rais wa nchi.
5. Rais huyu kwa mwezi matumizi yake hayazidi shilingi milioni moja laki
 nne za Kitanzania ambapo kwenye kuorodhesha kiwango cha kipato cha kila
 kiongozi kwa mwaka na mali binafsi ikiwa ni lazima nchini humo kwa 
viongozi mbalimbali wa serikali mwaka 2010, alikutwa na kiasi cha dollar
 $ 1,800 tu kiasi ambacho hakizidi shilingi milioni tatu za kitanzania.
6. Gari anayotumia ndio hiyo picha ya kwanza hapo juu ambayo ni ya mwaka 1987 aina ya Volkswagen Beetle.
8. Akiwa jela Mujica anasema hali ile ilimbadilishia mtazamo wake juu ya maisha na anakwambia ‘mimi naitwa rais maskini lakini mimi wala sihisi umaskini wowote,
 watu masikini ni wale ambao kazi yao ni kuishi maisha ya gharama ambayo
 inawasababisha kufanya kazi sana ili waendelee na maisha ya gahrama na 
kupata zaidi’
0 comments:
Post a Comment