Facebook

Monday 25 August 2014

Real Madrid yakubali Di Maria kujiunga Manchester United.


DIMARIAn_ROJOManchester United wamekamilisha mazungumzo na Real Madrid na kukubaliana kulipa Dau la Pauni Milioni 63.9 kumnunua Angel Di Maria ambayo ni rekodi kwa Uingereza.

Leo hii Di Maria anatarajiwa kutua Jiji la Manchester kwa mazungumzo ya mwisho na kujitayarisha kuikabili Burnley kwenye Mechi ya Ligi huko Turf Moor Jumamosi ijayo.

Ada hii ya Uhamisho wa Di Maria itavunja rekodi ya Ununuzi wa Bei ghali wa Fernando Torres ambayo Chelsea walilipa Pauni Milioni 50 kumnunua kutoka Liverpool Miaka Mitatu iliyopita.

Kwa mujibu wa Kituo cha TV cha Sky Sports, kupitia Mdadisi wao na Mtaalam wa Masuala ya Soka ya Spain, Guillem Balague, Man United walitoa Ofa ya Euro Milioni 60 na Real kutaka Euro Milioni 90 na hatimae kukubaliana Euro Milioni 80 ambazo ni sawa na Pauni Milioni 63.9.

Mara baada ya Leo kutoka Sare 1-1 na Sunderland huko Stadium of Light hapo jana, Meneja wa Man United, Louis van Gaal, aliulizwa kuhusu Di Maria na akajibu: “Klabu inapaswa kutangaza. Ikiwa mambo tayari tutakuja na kuwaambia safi! Kwa sasa hatusemi lolote!”

Alipoulizwa moja kwa moja kama angependa kumsaini Di Maria, Van Gaal alijibu ndiyo na kuongeza: “Pia nampenda Messi na nampenda Vidal na wapo Wachezaji wengi Duniani nawapenda lakini wote hawawezi kuja Manchester United!”

Huko Madrid hapo jana, Meneja wa Real Madrid, Carlo Ancelotti, amethibitisha kuondoka kwa Angel Di Maria na kusema alikwenda Kituo cha Mazoezi kuaaga wenzake.

0 comments:

Post a Comment