Facebook

Monday, 25 August 2014

Real Madrid yakubali Di Maria kujiunga Manchester United.


DIMARIAn_ROJOManchester United wamekamilisha mazungumzo na Real Madrid na kukubaliana kulipa Dau la Pauni Milioni 63.9 kumnunua Angel Di Maria ambayo ni rekodi kwa Uingereza.

Leo hii Di Maria anatarajiwa kutua Jiji la Manchester kwa mazungumzo ya mwisho na kujitayarisha kuikabili Burnley kwenye Mechi ya Ligi huko Turf Moor Jumamosi ijayo.

Ada hii ya Uhamisho wa Di Maria itavunja rekodi ya Ununuzi wa Bei ghali wa Fernando Torres ambayo Chelsea walilipa Pauni Milioni 50 kumnunua kutoka Liverpool Miaka Mitatu iliyopita.

Kwa mujibu wa Kituo cha TV cha Sky Sports, kupitia Mdadisi wao na Mtaalam wa Masuala ya Soka ya Spain, Guillem Balague, Man United walitoa Ofa ya Euro Milioni 60 na Real kutaka Euro Milioni 90 na hatimae kukubaliana Euro Milioni 80 ambazo ni sawa na Pauni Milioni 63.9.

Mara baada ya Leo kutoka Sare 1-1 na Sunderland huko Stadium of Light hapo jana, Meneja wa Man United, Louis van Gaal, aliulizwa kuhusu Di Maria na akajibu: “Klabu inapaswa kutangaza. Ikiwa mambo tayari tutakuja na kuwaambia safi! Kwa sasa hatusemi lolote!”

Alipoulizwa moja kwa moja kama angependa kumsaini Di Maria, Van Gaal alijibu ndiyo na kuongeza: “Pia nampenda Messi na nampenda Vidal na wapo Wachezaji wengi Duniani nawapenda lakini wote hawawezi kuja Manchester United!”

Huko Madrid hapo jana, Meneja wa Real Madrid, Carlo Ancelotti, amethibitisha kuondoka kwa Angel Di Maria na kusema alikwenda Kituo cha Mazoezi kuaaga wenzake.

Related Posts:

  • UHAMISHO WA WACHEZAJI ULIOKAMILIKA HADI HIVI SASA LIGI KUU UINGEREZA KLABU za Ligi Kuu England zipo kwenye heka heka kubwa za kusajili Wachezaji wapya kwa ajili ya Msimu mpya wa 2014/15 unaoanza Agosti 16 lakini Dirisha la Uhamisho litafungwa rasmi Septemba 1 Saa 7 Usiku kwa saa za Afr… Read More
  • Algeria yateua kocha mpya.   Christian Gourcuff ameteuliwa kuwa kocha mpya wa Algeria siku ya Jumamosi. Raia huyo wa Ufaransa anachukua nafasi ya Vahid Halilhodzic aliyewapeleka Mbweha wa Jangwani katika raundi ya pili ya Kombe la Dunia … Read More
  • Mourinho "Nimemaliza Usajili"   Boss wa Chelsea, Jose Mourinho amesema amemaliza kununua wachezaji msimu huu baada ya kukamilisha usajili wa beki wa kushoto Filipe Luis kutoka Atlètico Madrid. Luis ni mchezaji wa nne mpya kusajiliwa na Mouri… Read More
  • Nyota wa Nigeria asajiliwa West Brom.   West Brom wamemsajili mshambuliaji kutoka Nigeria Brown Ideye kwa kitita kinachodhaniwa kuwa pauni milioni 10. West Brom wametangaza kuwasili kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 akitokea Dynamo Kiev siku y… Read More
  • Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya. Fabio Borini, 23, anajiandaa kujiunga na Sunderland baada ya Liverpool kukubali ada ya pauni milioni 14 (Sky Sports), Baada ya kumchukua Filipe Luis siku ya Ijumaa, Chelsea wanazungumza na Atlètico Madrid kuhusu kums… Read More

0 comments:

Post a Comment