Facebook

Thursday, 22 May 2014

Ronaldo na Bale kushiriki fainali ya Ligi ya Mbingwa Ulaya

 

Mchezaji bora duniani mwaka huu Cristiano Ronaldo na mshambulizi aliyegharimu kitita kikubwa zaidi duniani Gareth Bale watakuwepo katika timu ya Real Madrid itakayochuana na Atletico Madrid katika fainali ya kuwania kombe la mabingwa barani Uropa jumamosi hii.
Ronaldo, 29, alikuwa amekosa kucheza mechi mbili akiuguza jereha sawa na mshambulizi Gareth Bale, 24, ambaye hakushiriki katika mazoezi siku ya jumanne.
Wawili hao kwa ushirikiano wamiefungia Real Madrid mabao 68 msimu huu.
Kocha Carlo Ancelotti, ambaye anapania kuwa mkufunzi wa pili katika historia ya mchuano huu kuwahi kushinda taji la ubingwa barani Ulaya mara tatu amethibitisha kuwa nyota hao wawili wakali kwa mashambuli watakuwepo
Ronaldo atacheza dhidi ya Atletico Madrid
Lisbon huku akiongezea kuwa anasubiri ithibati ya muuguzi wa timu kuhakiki kuwepo kwa mlinzi Pepe na mshambulizi Karim Benzema.
Benzema alijeruhiwa Real ilipoibana Espanyol 3-1 huku Pepe akisalia kwenye bench kwa zaidi ya majuma mawili sasa.
Real Madrid inapania kutawazwa mabingwa wa Uropa iwapo watawalaza washindi wapya wa ligi kuu ya Uhispania Atletico Madrid mbali na kusitisha ukame wa miaka 12 wa kombe hilo lenye umaarufu barani Uropa.
Aidha fainali hii baina ya mahasimu hao wa jadi wanaootokea mji wa Madrid itakuwa ya kwanza katika historia ya kombe hili kujumuisha wapinzani wa ligi ya nyumbani.
Atletico wamechuana dhidi ya Real Madrid mara nne msimu huu ,Real ikishinda mechi za kuwania kombe la Spanish kwa mabao 5-0 huku Atletico ikiibuka na ushindi katika mechi za ligi ya Uhispania .
Atletico kwa upande wake inasubiri kujua hali ya siha ya mshambulizi wake Diego Costa ambaye alijeruhiwa mapema katika mechi ya kuamua mshindi wa la Liga dhidi ya Barcelona mwishoni mwa juma.

Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua kila kitakachokuwa kinajiri kuelekea katika pambanao la fainali ya UCL baina ya  Atletico Madrid na Real Madrid

Related Posts:

  • Liverpool vs Chelsea:LIVE COMMENTARYLIGI KUU ENLGAND: LEO KUANZIA SAA 9 DAK 45 MCHANA LIVERPOOL v CHELSEA VIKOSI: Liverpool: Mignolet; Johnson, Skrtel, Lovren, Moreno: Can, Henderson, Gerrard; Coutinho, Sterling, Balotelli. Kiba: Brad Jones, Toure, Lambert, Lal… Read More
  • Mrundi aitwa kikosi cha Uingereza   Mshambuliaji wa klabu ya West Brom ya Uingereza, Saido Berahino ametajwa katika kikosi cha England kwa mara ya kwanza na meneja Roy Hogson. Berahino, 21, huenda akacheza mechi dhidi ya Slovenia ya kufuzu Euro 201… Read More
  • UCHAMBUZI:LIVERPOOL vs CHELSEATAREHE 8 NOVEMBA 2014 LIGI KUU YA UINGEREZA LIVERPOOL  V  CHELSEA ANFIELD Saa 9:45 alasiri: HABARI ZA KILA TIMU KWA UFUPI: Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard anatarajiwa kuanza kwenye mechi ya Leo baada ya kuanzia… Read More
  • BantuTz LIVESTREAMING::->Liverpool Vs ChelseaAngalia live kupitia Computer au Tablet yako mechi kati ya Liverpool dhidi ya Chelsea Utaangalia mechi hiyo bila kukwama au kukatika kwa matangazo ya mechi hiyo hata kidogo. Utafurahia kuangalia mechi hiyo kama utatumia Compu… Read More
  • Habari za Michezo Kutoka Bongofun.blogspot.com ARSENAL WATAWALA KIKOSI CHA ENGLAND,MRUNDI BERAHINO NAYE NDANI Wayne Rooney na Wilshere                     &nbs… Read More

0 comments:

Post a Comment