Facebook

Sunday, 18 May 2014

Wanamgambo wavamia kiwanda Cameroon


Familia ya raia wa Ufaransa iliotekwa nyara nchini Cameroon.
Maafisa nchini Cameroon wanasema kuwa kumekuwa na shambulizi katika kiwanda kimoja cha raia wa Uchina kazkazini mwa taifa hilo.
Ubalozi wa Uchina nchini Cameroon umesema kuwa takriban watu kumi wametoweka huku mtu mmoja akijeruhiwa katika kile ilichoelezea kama shambulizi kutoka kwa watu wasiojulikana.
Kisa hicho kimetokea karibu na mpaka wa kazkazini mashariki mwa Nigeria ambayo ndio ngome kuu ya kundi la wanamgambo wa kiislamu wa Boko Haram.
Wanamgambo hao wamefanya mashambulizi kadhaa nchini Cameroon .
Mwaka uliopita waliiteka nyara familia moja ya Ufaransa kabla ya kuiwachilia huru baada ya miezi miwili.

Related Posts:

  • WAPENZI WA JINSIA MOJA WAFUNGA NDOA BAADA YA KUISHI PAMOJA MIAKA 72Zaidi ya miongo sabini baada ya kuanza uhusiano wa kimapenzi, Vivian Boyack na Alice "Nonie" Dubes wamefunga ndoa. Boyack, 91, na Dubes, 90, walifunga ndoa rasmi Jumamosi iliyopita, limeripoti gazeti la Quad City Times. "Sher… Read More
  • Nyama ya Kiboko yawaletea maafa Afrika KusiniWatu kumi walikanyagwa na gari lililokuwa linakwenda kwa mwendo wa kasi walipokuwa wanajaribu kujipatia angalau kipande cha nyama ya Kiboko mwishoni mwa wiki. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation. Kiboko huyo … Read More
  • Wafungwa wapigwa risasi mahakamani Afrika Kusini.Wafungwa wawili wamepigwa risasi walipokuwa wakijaribu kutoroka kutoka katika mahakama moja nchini Afrika Kusini. Afisa mmoja kutoka wizara ya sheria aliambia chama cha wanahabari nchini humo kwamba wafungwa waliokuwa wanasub… Read More
  • Tahadhari kuhusu gesi za sumuMkuu wa shirika la utabiri wa hali ya anga la Umoja wa Mataifa Michel Jarraud, ametoa tahadharti kuwa dunia nzima inapaswa kushughulikia mabadiliko ya hali ya anga haraka iwezekanavyo la sivyo muda unakwisha. Takwimu mpya kut… Read More
  • Congo watangaza hatua mpya za kupambana na Ebola.Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza hatua mpya za kupambana na ugonjwa wa Ebola wiki 3 baada ya ugonjwa huo kuwauwa watu 32 miongoni mwa 59 waliombukizwa na virusi hivyo.Waziri wa Afya nchini humo amesema … Read More

0 comments:

Post a Comment