Habari zilizotufikia hivi punde kutoka mkoani Mwanza ni kwamba kumetokea machafuko makubwa sana baada ya Jeshi la Polisi kupambana na Wamachinga.
Ilikuwa ni mida ya asubuhi ambapo Jeshi la polisi lilikuwa limeshatoa
tamko kwa wamachinga wanatakiwa kuondoka maeneo ya Stndi ya Tanganyika
na Mtaa wa Makoroboi na kutofanya biashara katika maeneo hayo na
kandokando mwa barabara katika jiji hilo linaloongoza kwa usafi nchini.
Wamachinga
walipingana na tamko hilo na kuamua kugoma kuondoka maeneo yao ya
kufanyia kazi hususan maeneo ya Tanganyika standi na Mtaa wa
Makoroboi.Baada ya kugoma waendesha bodaboda nao wakaamua kuingilia kati
huku wao wakiwaunga mkono wamachinga.
Baada ya mgomo huo askari wa Jeshi la Polisi mkoani mwanza waliamua
kwenda kuwatawanya wamachinga na waendesha bodaboda ndipo vurugu
zilizpoanza kwani wamachinga walianza kuwarushia polisi
mawe,miti,vipande vya kokoto na vyuma chakavu.
Vilevile wamachinja walienda hadi eneo yalipo makao makuu ya manispaa ya Jiji la mwanza na kulichoma moto gari la manispaa.
Kutokana na vurugu hizo jeshi la Polisi liliongezewa nguvu na Kikosi
maalum cha kutuliza ghasia (FFU) ambao wao waliwatawanya wamachinga na
Waendesha Bodaboda kwa kutumia mabomu ya machozi.
Huku baadhi ya wamachinga wakikamatwa na kupewa kipigo kikali.
Baada ya kikosi maalum cha kutuliza ghasia kufika eneo hilo wamachinga
waliamua kukimbilia sehemu mablimbali hasa milimani na Ziwani.
Kikosi maalum cha kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa wanawasili eneo la tukio-Stand ya Tanganyika
Kikosi maalum cha kutuliza Ghasia (FFU) wakiwa wanawasili eneo la tukio-Stand ya Tanganyika
Mtaa
wa Makoroboi ukiwa tulivu baada ya kuwasili kwa kikosi maalum cha
kutuliza Ghasia (FFU) huku wamachinga wakiwa wamekimbia eneo hilo.
Mmachinga mmoja ambaye kamera yetu ilimnasa akiwa amekimbilia ziwani kuhofia kukamatwa na kupewa kipigo kikali kwa askari.
Wamachinga
wakiwa wametanda katika maeneo yao ya kufanyia biashara wakiwa
wamekaidi tamko la Serikali la kuwataka kuhama katika maeneo yao ya
kufanyia biashara.
Baada
ya kikosi cha kutuliza Ghasia kufika maeneo hayo na kurusha mabomu ya
machozi wametoa tamko kwamba wamachinga waache fujo la sivyo
watachukuliwa hatua kali wale wote watakao kamatwa kwa kiuka tamko hilo.
Tuko katika maboresho hivi karibuni
blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za
kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano
mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia
kupitia www.bantutz.com...
0 comments:
Post a Comment