Facebook

Tuesday, 17 June 2014

Nigeria na Iran zatoka sare.


Timu ya Iran na Nigeria zilitoka sare ya suluhu bin suluhu , katika mechi yao ya kundi F huko Curitiba, kwenye fainali ya kombe la dunia siku ya Jumatatu.
Timu hiyo ya Carlos Queiroz ilionekana kuwa ngumu kushindwa tangu mwanzoni.
Super Eagles ya Nigeria,ambao walikua na rekodi nzuri katika michuano ya kufuzu kwa kombe la dunia walishindwa kupenya safu ya ulinzi ya Iran.
Hii ilikua sare ya kwanza tasa katika michuano ya kombe la dunia mwaka 2014.
Timu zote mbili zilijaribu kupata nafasi ya kufunga bao lakini hakuna iliyofaulu.
Iran ilipoteza nafasi ya kufunga bao pale ambapo kipa wa Nigeria, Vincent Enyeama alipouzuia mkwaju wake Reza Ghoochannejad.
Mabingwa hao wa bara Afrika mwaka 2013, walitarajiwa kushinda mchuano huo lakini timu ya Iran iliwapatia changamoto si haba.
Matokeo haya yanaipa timu ya Argentina uongozi wa kundi hilo baada ya kuishinda timu ya Bosnia-Herzegovina, 2-1, siku ya Jumapili.
Timu ya Iran itakutana na Argentina siku ya Jumamosi, huko Belo Horizonte, nayo Nigeria kuiandaa kukabiliana dhidi ya Bosnia kule Cuiaba.
Nigeria ilimiliki mchuano huo katika muda wote wa dakika 90, lakini hawakufaulu kuwashinda wa Irani.
Mkwaju wake Ghoochannejad na ule wa Ahmed Musa ndizo zilizokua nafasi nzuri za kufunga bao katika kipindi cha kwanza.
Katika kipindi cha pili, Shola Ameobi alizuiwa mara mbili na mlinzi wa Iran, Mehrdad Poolani.

Victor Moses ndiye aliyepata nafasi ya kwanza ya Nigeria kupata uongozi lakini mkwaju wake hafifu ulikamatwa na kipa wa Iran Reza Haghighi.
Kipa wa Iran Haghighi, asiye na uzoefu mkubwa katika mechi za kimataifa alionekana kutishika kila wakati washambulizi wa Super Eagles waliposhambulia lango lake na aliponea katika dakika ya saba kutokana na mkwaju wa kona.
Kenneth Omeruo alitia mpira wavuni lakini refa tayari alikua ameshapuliza kipenga kuonyesha kuwa kipa, Haghighi alikua amechezewa visivyo na John Obi Mikel.

Emmanuel Emenike alijaribu katika upande wa kushoto, lakini Pejman Montazeri alikua kizuizi katika upande huo pia.
Katika kipindi cha pili, Iran ilianza kuonyesha kujiamini na kuanzisha mashambulizi dhidi ya lango la Nigeria.
Mchuano huu ulielekea kuonekana kuwa hafifu na hakuna timu iliyoonyesha ukakamavu wa kuchuana na Argentina ama Bosnia.
Shola Ameobi aliingia katika nafasi yake Victor Moses katika dakika ya 52 na akaja karibu kuipatia Nigeria bao la kwanza baada ya kupewa pasi na Ramon Azeez.
Nigeria tena walikaribia kupata bao katika dakika za mwisho kupitia kwake Ogenyi Onazi.
Hata hivo mchuano huo ulitimia kuisha kwa sare tasa.


Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

  • MANCHESTER UNITED WAPO TAYARI KUMLIPA TYLER BLACKETT £ 50,000 KWA WIKI-Uongozi wa Manchester United umetangaza rasmi kwamba wapo katika hatua ya mwisho ya kuuboresha mkataba wa beki kinda mwenye umri wa miaka 20,Tyler Blackett ili aendelee kuwepo kikosini hapo baada ya kuonekana bora na kocha V… Read More
  • Majeruhi wazidi kuongezeka Arsenal.   Kwa sasa tuna wachezaji kumi wa kikosi cha kwanza wapo nje kwa majeruhi. Katika mchezo wa jana wa timu ya taifa Uingereza kufuzu Euro 2016 Danny Welbeck alitonesha enka yake na kutolewa nje dakika 10 kabla ya mpi… Read More
  • Mechi mbalimbali zitakazochezwa leo hii. LEO IJUMAA MECHI ZA KUFUZU EURO 2016 9:45 PM - Latvia vs Iceland 9:45 PM - Netherlands vs Kazakhstan 9:45 PM - Turkey vs Czech Republic 9:45 PM - Belgium vs Andorra 9:45 PM - Cyprus vs Israel 9:45 PM - Wales vs Bosnia-Herzeg… Read More
  • MATOKEO YA MECHI ZA KUFUZU EURO 2016 Group C Slovakia (Kucka '17, Stoch '87) 2-1 Spain (Alcacer 83) Belarus 0-2 Ukraine (Martynovich '82 og, Sydorchuk '90) Macedonia (Trajkovski '20, Jahovic '66,Abdurahimi '90) 3-2 Luxembourg (Bensi '39, Turpel '44) Group E Engl… Read More
  • Tanzania yaifumua Benin 4-1Taifa Stars imeitungua Benin kwa mabao 4-1 katika mechi ya kitarafiki ya kimataifa iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Stars yalifungwa na wachezaji wake wawili wanaokipiga nchini na wawili w… Read More

0 comments:

Post a Comment