Facebook

Monday, 2 June 2014

Picha: Mazishi ya Bi Shida Salum, mama yake Zitto Kabwe – Kigoma

Jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum likiwekwa vizuri kwa ajili ya ibada kisha kupelekwa kwenye makazi ya milele.

Zifuatazo ni baadhi ya picha kutoka Kigoma katika mazishi ya Bi Shida Salum, mama mzazi wa Zitto Kabwe. Bi Shida alifariki Jumapili asubuhi katika hospitali ya AMI jijini Dar Es Salaam baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum likishushwa ili kuhifadhiwa kwenye mapumziko yake ya milele. Picha na JamiiForums.
Jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum likiwasili nyumbani kwa familia kwa ajili ya shughuli za mazishi.
Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe (CHADEMA) akiwa na baadhi ya wazee wa Kigoma kwenye maandalizi ya mazishi ya mama yake mzazi, Bi Shida Salum, aliyefariki Jumapili, Juni 1 jijini Dar Es Salaam.
Mbunge wa jimbo la Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe akiwa na wabunge wenzie na baadhi ya wazee wa Kigoma kwenye maandalizi ya mazishi ya mama yake mzazi Bi Shida Salum aliyefariki Juni 1 katika hospitali ya AMI jijini Dar Es Salaam.
Zitto Kabwe akisalimiana na baadhi ya wageni waliokuja kumpa pole.
Zitto Kabwe (mwenye kanzu nyeusi) akipewa pole na wageni waliofika kumfariji katika msiba wa mama mzazi.
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakionekana kuumizwa na kifo cha mama yake Zitto Kabwe.
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakionekana kuumizwa na kifo cha Bi Shida Salum, mama yake Zitto Kabwe.

Jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum likiombewa na baadhi ya viongozi wa kiislamu Kigoma Kaskazini.
Kiongozi wa kidini akitoa mawaidha mbele ya jeneza lenye mwili wa marehemu Bi Shida Salum, mjini Kigoma.
Halaiki ya wakazi wa Kigoma Kaskazini wakisindikiza jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum (halionekani pichani) kwenda kupumzishwa kwenye makazi yake ya milele mchana huu Kigoma.
Umati wa wakazi wa Kigoma wakisindikiza jeneza lenye mwili wa marehemu Shida Salum (halionekani pichani) kwenda makaburini, Jumatatu mchana. 


Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari,tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment