Facebook

Sunday, 22 June 2014

Urusi yaweka jeshi tayari kwa vita na Ukraine

Rais Putin ameagizwa wanajeshi wake kufanya mazoezi na kuwa tayari kwa vita.
Rais Putin ameagizwa wanajeshi wake kufanya mazoezi na kuwa tayari kwa vita.
Rais Vladimir Putin wa Urusi ameviweka vikosi vyake vilivyoko nchini humo katika hali ya “tahadhari kamili ya vita” na kuwaamuru wanajeshi 65,000 katika eneo hilo kufanya luteka za kijeshi za wiki moja kuwa tayari kwa vita.
Waziri wa Ulinzi wa Urusi, Sergei Shoigu, amesema mazoezi hayo ya kijeshi ya angani na ardhini katika maeneo ya milima ya Volga na Ural yatafanyika kuanzia Jumamosi Juni 21 hadi Juni 28.
Jumuiya ya Kujihami ya NATO imesema mapema wiki hii kwamba Urusi imerudia tena kurundika wanajeshi wake kwenye mpaka na Ukraine ambapo waasi wanaotaka kujitenga wamekuwa wakipambana na vikosi vya serikali kwa wiki kadhaa katika mzozo uliogharimu maisha ya watu 300 na kuwapotezea makaazi wengine 34,000.
Kusitisha uhasama
Hatua hizo za kijeshi zinakuja siku moja baada ya Rais Petro Poroshenko wa Ukraine kutangaza wiki moja ya usitishaji wa mapigano na waasi wanaoiunga mkono Urusi mashariki ya nchi hiyo ikiwa ni sehemu ya mpango wa amani wa vipengele vinne ambao pia unajumuisha msamaha na ahadi ya kufanyika kwa marekebisho ya katiba.
Serikali ya Urusi imeishutumu mpango huo wa Poroshenko kuwa ni “amri” ambao hautopelekea kupatikana kwa ufumbuzi wowote ule na waasi wameukataa wito wake wa kuwataka wasalimishe silaha zao.

Related Posts:

  • Watu 20 wauawa katika mashambulio mawili katika Pwani ya Kenya.   Watu wasiopungua 20 wameuawa katika mashambulio mawili katika kaunti mbili kwenye pwani ya Kenya usiku wa kuamkia Jumapili. Watu walioshuhudia matukio hayo wamesema, watu wenye silaha nzito walishambulia eneo … Read More
  • Marekani yachukizwa na hatua ya Israel Ghasia kati ya Palestina na Israel Marekani imesema kuwa ina wasiwasi mwingi kwamba maafisa wa Polisi wa Israel wamempiga vibaya kijana mmoja raia wa Marekani. Idara ya maswala ya kigeni imesema kuwa inashtumu utumij… Read More
  • Watu zaidi ya 50 wauawa Uganda.   Watu wasiopungua 50 wameuawa baada ya watu wenye silaha kushambulia vituo vya polisi na kambi za jeshi nchini Uganda, kwa mujibu wa jeshi. Miongoni mwa waliokufa ni washambuliaji 41 na polisi pamoja na raia 17… Read More
  • 29 wauawa katika shambulizi, kenya Wizara ya maswala ya ndani nchini Kenya inasema kuwa takriban watu thelathini wameuawa katika mashambulizi mawili tofauti katika makaazi ya pwani ya ke… Read More
  • Vita kali yazuka Yemen. Ripoti kutoka Yemen zinasema kuwa kumekuwa na vita vikali kati ya jeshi la taifa hilo na waasi wa ki-shia kazkazini mwa taifa hilo kufu… Read More

0 comments:

Post a Comment