Facebook

Sunday, 18 May 2014

Atletico Madrid Mabingwa wa La Liga 2014

Photo: ¡¡¡Campeones!!! Orgulloso de este equipo y de nuestra afición #AúpaAtleti


Wachezaji wa Atletico Madrid wakishangilia goli
Atletico Madrid imenyakua kombe la ligi kuu ya Hispania La liga baada ya kutoka sare ya 1 – 1 dhidi ya Barcelona na hivyo kumaliza ligi ikiwa na pointi 90 huku Barcelona ikishika nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 87.
Real Madrid iliyoshinda mechi yake dhidi ya Espanyol kwa 3 - 1 ikishika nafasi ya tatu kwa kumaliza ligi ikiwa na pointi 87 lakini ikizidiwa na Barcelona kwa tofauti ya goli moja.
Barcelona wana tofauti ya magoli 67 wakati Real Madrid ikiwa na tofauti ya magoli 66.
Katika mechi hiyo ya Barcelona dhidi Atletico Madrid ambayo ilikuwa ni ya kuamua ni timu ipi itanyakua ubigwa wa La Liga msimu huu, Barcelona ndio waliokuwa wa kwanza kuutikisa wavu wa Atletico Madrid kwa goli lililofungwa na Alexis Sanchez katika ya 34 kipindi cha kwanza.
Baadae Atletico Madrid walikuja juu na kuanza kulishambulia goli la Barcelona ambapo Diego Godin katika dakika ya 49 kipindi cha pili aliIsawazishia timu yake kwa goli safi alilolipachikwa wavuni kwa njia ya kichwa na hivyo kufanya mechi hiyo imalizike kwa jumla ya goli 1 - 1 .
Atletico Madrid inakuwa mabingwa wa La Liga tangu baada ya kulikosa kombe hilo tangu mwaka 1996.
 
 

Related Posts:

  • Daley Blind "Siko tayari kulinganishwa na Roy Keane"  Blind alisema ameyazoea maisha ya Manchester United kwa muda mfupi,lakini asisitiza kuwa nimapema sana kumlinganisha na Roy Kean, Blind alisema "tusiende mbali sana,maendeleo yangu ni mazuri kwa sasa lakini ndo kwanz… Read More
  • Ronaldo kuzeekea Real Madrid   Cristiano Ronaldo hana nia ya kurejea Manchester United na atamalizia kucheza soka yake Real Madrid, amedai wakala wake Jorge Mandes.  Ronaldo, 29, tayari amefunga magoli 15 msimu huu, ikiwemo kufikisha … Read More
  • MANCHESTER UNITED WAPO TAYARI KUMLIPA TYLER BLACKETT £ 50,000 KWA WIKI-Uongozi wa Manchester United umetangaza rasmi kwamba wapo katika hatua ya mwisho ya kuuboresha mkataba wa beki kinda mwenye umri wa miaka 20,Tyler Blackett ili aendelee kuwepo kikosini hapo baada ya kuonekana bora na kocha V… Read More
  • MATOKEO YA MECHI ZA KUFUZU EURO 2016 Group C Slovakia (Kucka '17, Stoch '87) 2-1 Spain (Alcacer 83) Belarus 0-2 Ukraine (Martynovich '82 og, Sydorchuk '90) Macedonia (Trajkovski '20, Jahovic '66,Abdurahimi '90) 3-2 Luxembourg (Bensi '39, Turpel '44) Group E Engl… Read More
  • Mechi mbalimbali zitakazochezwa leo hii. LEO IJUMAA MECHI ZA KUFUZU EURO 2016 9:45 PM - Latvia vs Iceland 9:45 PM - Netherlands vs Kazakhstan 9:45 PM - Turkey vs Czech Republic 9:45 PM - Belgium vs Andorra 9:45 PM - Cyprus vs Israel 9:45 PM - Wales vs Bosnia-Herzeg… Read More

0 comments:

Post a Comment