Facebook

Friday 16 May 2014

Nigeria yapuuza matakwa ya Boko Haram

Nigeria yapuuza Boko Haram
Rais wa Nigeria ametupilia mbali matakwa ya la kundi la kiislam la Boko Haram kwamba serikali iwaachilie huru wafungwa wa kundi hilo ndipo litawachilia wasichana zaidi ya 200 waliiotekwa na kundi hilo.
Serikali ya Nigeria imesema iko tayari kwa mazungumzo na kundi la wanamgambo la Boko Haram.
Hatahivyo inaendelea kubainika kuwa kuna mipaka ambayo serikali inaaishiria kuwa haitavuka.
Kwa mujibu wa waziri wa Uingereza anayehusika na masuala ya Afrika Mark Simmonds aliye ziarani nchini Nigeria, Rais Goodluck Jonathan amemwambia wazi kuwa serikali haitakubali pendekezo la Boko Haram kubadilishana wafuasi wake waliofungwa jela na serikali na wasichana waliotekwa nyara na kundi hilo.
Lakini hilo ndio sharti pekee ambalo kiongozi wa Boko Haram , Abubacar Shekau ametoa.
Nigeria yapuuza matakwa ya Boko Haram kabla ya kuwaachilia wasichana.
Haijulikani sasa mazungumzo kati ya serikali na kundi hilo yatahusu nini baada ya pande zote mbili kushikilia misimamo mikali.
Waziri huyo wa Uingereza amesema baada ya mzozo uliopo kutatuliwa kuna haja ya kuwajibisha waliotekeleza utekaji nyara huo ambao ni , Abubacar Shekau na wafuasi wa Boko Haram.
Tamko hilo pia linaongezea uzito katika msimamo wa serikali na hivyo kutilia shaka uwezekano wa mzozo huo kutatuliwa kwa haraka.

0 comments:

Post a Comment