Facebook

Thursday, 1 May 2014

Nigeria:Maandamano dhidi ya serikali................

Maandamano kuhusu wasichana waliotekwa
Maandamano makubwa ya kwanza yanatarajiwa kufanyika katika mji mkuu wa Nigeria- Abuja baadaye leo watu wakiitaka serikali kuchukua hatua zaidi kuwanusuru wasichana 200 wa shule waliotekwa nyara na wanamgambo wa kiislam .
Wasichana hao walichukuliwa kutoka shule yao ya malazi iliyopo katika eneo lisiloweza kufikiwa kwa urahisi kaskazini mashariki mwa nchi zaidi ya wiki mbili zilizopita.
Waandalizi wa maandamano hayo wanaita serikali kuelekeza juhudi zao kwa wasichana waliopotea .
Mpango ni kuandamana hadi bungeni na kwa mshauri wa taifa wa masuala ya usalama na kuwasilisha barua ya kutoa wito wa kufanyika kwa juhudi zaidi kuwanusuru wasichana hao.
Mwanaharakati mmoja wa kijamii amesema katika nchi nyingine yoyote ile suala la kutekaji nyara wa wasichana hao wengi lingekuwa ni mjadala wa kila siku .
Lakini serikali ya Nigeria imekuwa ikikabiliwa na ukosoaji mkubwa kwa kukaa kimwa huku wazazi wenye shauku wakisailia kuwa gizani kuhusu nini kinachoendelea kuhusiana na wasichana wao.
Huenda kwa kuhisi hilo rais wa Seneti , David Mark, sasa amezungumza. Amewatolea wito watekaji kuawaachilia mara moja wasichana bila masharti na akasema bila shaka taifa letu liko vitani .

Related Posts:

  • HATIMAYE KIONGOZI WA AL SHABAB AUAWA Aliyekua kiongozi mkuu wa Alshabab Ahmed Abdi Godane ameripotiwa kuuawa!! Habari kutoka katika idara kuu ya ulinzi ya marekani PENTAGONI imesema kua kuuawa kwa kiongozi huyo mwanzilishi wa kikundi ambacho kimekua mwiba mkali… Read More
  • Boko Haram wazuia watu kuzika maiti Wapiganaji wa Boko Haram wamesababisha maafa Kaskazini ya Nigeria ngome yao ya vita Taarifa za kutisha zimeibuka kutoka mjini Bama moja… Read More
  • Damu ya waliopona Ebola kutibu Wagojnwa wengine. Shirika la afya duniani WHO limesema kuwa damu ya watu ambao wamepona ugonjwa wa Ebola inaweza kutumiwa kuwatibu wagonjwa wengine. Katika mkutano mjini Geneva, wataalam wa shirika hilo walikubaliana kwamba hii itakuwa njia ya… Read More
  • KESI YA KENYATTA YAPIGWA KALENDAWaendesha mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC iliyopo The Hague wameomba kesi ya Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta kuahirishwa tena. Bwana Kenyatta anashtakiwa kwa makosa dhidi ya ubinaadam, lakini upande wa mashtaka umes… Read More
  • Alshabaab wathibitisha kifo cha kiongozi wao,Godane Kundi la wapiganaji wa kisomali Al-shabaab limethibitisha kuwa kiongozi wake Ahmed Abdi Godane aliuawa siku ya jumatatu katika shambulizi la angani lililotekelezwa na wanajeshi wa Marekani. … Read More

0 comments:

Post a Comment