Friday, 2 May 2014
Sheikh Ponda azidi kusota rumande......!!!
Kesi inayomkabili kiongozi wa Taasisi ya Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda imeendelea kupigwa kalenda katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mkoa wa Morogoro.
Ilielezwa mahakamani hapo jana kuwa kesi hiyo haiwezi kusikilizwa kwa sasa kwa kuwa jalada lake bado halijarudi kutoka Mahakama Kuu, Kanda ya Dar es Salaam.
Sheikh Ponda anakabiliwa na mashtaka matatu ambayo ni kutotii amri halali ya iliyotolewa na Mahakama ya Kisutu, kutoa maneno yenye kuharibu imani za dini na kushawishi watu kutenda kosa, makosa ambayo anadaiwa kuyatenda Agosti 10 mwaka jana katika eneo la Uwanja wa Ndege Manispaa ya Morogoro.
Baada ya kutajwa kwa kesi hiyo, Hakimu Mkazi Mfawidhi Mary Moyo alisema kesi hiyo itaendelea kutajwa mpaka jalada hilo lililoitishwa Mahakama Kuu Oktoba 15 litakaporudishwa Mahakama ya Morogoro.
Sheikh Ponda alifikishwa mahakamani hapo jana chini ya ulinzi mkali wa polisi waliokuwa na sihala za moto, mabomu ya machozi na mbwa huku wafuasi wake wakizuiwa nje ya uzito wa mahakama hiyo.
Upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Wakili wa Serikali, Lilian Lutabula aliyeshirikiana na mwendesha mashtaka wa polisi, Zabron Msusi wakati upande wa utetezi uliwakilishwa na wakili Josephine Jackson kwa niaba ya wakili Bathoromeo Tarimu anayemtetea Sheikh Ponda.
Baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo, mshtakiwa Ponda alirudishwa rumande ambako ataendelea kupafanya kuwa maskani yake hadi Mei 5 mwaka huu kesi hiyo itakapoendelea kutajwa mahakamani hap
Related Posts:
Silaha nzito za kivita zakamatwa Kibondo-Kigoma. Zaidi ya risasi mia tano na bunduki moja ya kivita aina ya smg zimekamatwa baada ya polisi kufanya ukaguzi katika basi aina ya hiace lililokuwa likisafiri kutoka wilayani kasulu kwenda kibondo mkoani kigoma. … Read More
CHADEMA yaibwaga CCM serikali za mitaa SumbawangaChama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA mkoani Rukwa kimeshinda kwa kishindo kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, uliofanyika jana kwenye kata Tano za manispaa ya Sumbawanga, kwa kushinda viti 38 kati ya viti vya mitaa 44.… Read More
Waethiopia 13 wakamatwa wakisafirishwa Morogoro Jeshi la polisi mkoa wa Morogoro limewakamata wahamiaji haramu 13 kutoka nchini Ethiopia wakiwa kwenye gari ndogo aina Prado katika kijiji cha Lusanga Turiani wilayani Mvome… Read More
Vurugu Ilula Mkoani Iringa, Mwananchi afariki, Kituo cha Polisi chachomwa moto !Ni baada ya Polisi Kuuwa Raia.Inasemekana polisi walivamia eneo la kilabuni na kuanza kupiga kila raia na kusababisa kifo cha huyo mama muuza Pombe za kienyeji. Kosa ni kufungua kilabu cha Pombe kabla ya muda ulioruhusiwa … Read More
BantuTz MAGAZETINI:-SOMA KILICHOANDIKWA KATIKA MAGAZETI YOTE YA LEO FEBRUARI 25BantuTz MAGAZETINI:Ni miongoni mwa huduma bora kabisa tunazozitoa ili wewe mdau wa Bantu usipitwe na habari,stori au taarifa yoyote ile.Tunakuletea kila tunachokipata kwa wakati na muda muafaka.Soma kilichoandikwa katika ku… Read More
0 comments:
Post a Comment