Facebook

Saturday 24 May 2014

Tajiri ahukumiwa kifo nchini China


Tajiri mmoja anayeaminika kuwa mshirika wa aliyekuwa mkuu wa ujasusi nchini China Zhou Yongkang, amehukumiwa kifo.
Mahakama imewapata na hatia Liu Han na kakake Liu Wei ya kupanga mauaji ya aina ya kimafia.
Wanaume hao walikuwa miongoni mwa kikundi cha watu 36 walioshitakiwa na makosa sawa na hayo.
Hukumu dhidi ya Liu Han inaaminika kuwa sehemu ya mpango wa serikali kupambana na ufisadi.
Mahakama ilisema kuwa Liu Han alikuwa amefaidika kifedha kutokana na vitendo vya uhalifu.
Pia katika matukio mengi walifanya mauaji na vitendo vya uhalifu ambavyo waliwadhuru watu na hata kuwazuilia watu kinyume na sheria.
Kwa mujibu wa mahakama Bwana Liu aliendesha shughuli zake kwa kusaidiwa na maafisa kadhaa wa serikali ili kuweza kudhibiti mashine za michezo katika mkoa wa Guanghan .
Liu, ambaye ni mkuu wa zamani wa kampuni ya madini ya Sichuan Hanlong Group, aliorodheshwa katika nafasi ya 148 kwa utajiri wake duniani na jarida la Forbes mwaka 2012.
Kampuni yake iliwahi kujaribu kutaka kuinunua kampuni ya madini ya Australia Sundance Resources Ltd ingawa hilo halikufanyika.
Kesi hii bila shaka inazua maswali kadhaa kwa viongozi wa kisiasa nchini China.
Huenda mkuu wa zamani wa ujasusi Zhou Yongkang pia akashitakiwa kwa kushirikiana na Liu.
Ikiwa jambo hilo litafanyika, hesi dhidi yake itakuwa ya madai mabaya zaidi ya ufisadi kuwahi kushuhudiwa katika historia ya china.

0 comments:

Post a Comment