Facebook

Wednesday, 18 June 2014

Kundi la Al Shabaab lakiri kufanya mashambulizi Kenya

Watu zaidi ta arobaini na tano wameuawa katika mashambulizi ya Mpeketoni
Kundi la wapiganaji wa Al Shabaab nchini Somalia, limekiri kufanya mashambulizi katika eneo la Mpeketoni karibu na Lamu, Pwani ya Kenya.
Mashambulizi hayo yalisababisha vifo vya watu 49.
Huku wakikiri shambulizi hilo wametoa onyo kwa watalii kukoma kuja Kenya.
Taarifa ya kundi hilo ilisema kuwa shambulizi hilo lilikuwa la kulipiza kisasi dhidi ya serikali ya Kenya kwa kufanya msako dhidi ya waisilamu kwa njia ya kuwafunga kiholela na kuwaua wahubiri wa kiisilamu.
Baadhi ya walioshuhudia mashambulizi hayo wamearifu kuwa wameona maiti kadhaa na majeruhi wengi japo Polisi hawajathibitisha ni watu wangapi wameuawa.
Mji wa Mpeketoni uko umbali wa kilomita mia moja kutoka eneo la mpakani na Somalia.

Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment