Facebook

Monday, 16 June 2014

Kundi lenye msimamo mkali la ISIS limechapisha Picha za mauaji Iraq !


Vuguvugu la Sunni lenye msimamo mkali la ISIS ambalo limeteka maeneo ya Kaskazini mwa Iraq limesambaza picha ambazo zinaonyesha jinsi wapiganaji wake walivyoangamiza idadi kubwa ya wanajeshi wa Iraq.
Picha zinazosambazwa kupitia internet zinaonyesha miili ya watu iliyosongamana ndani ya mtaro ikiwa imepelekwa hapo kwa kutumia malori.
Wapiganaji wa ISIS wanaonekana wakibeba bendera nyeusi ya huku wakichoma miili hiyo na kulazimisha mateka kulala chini.

ISIS yachapisha picha za mauaji ya majeshi ya Iraq .
Msemaji wa jeshi nchini mjini Baghdad amesema anaamini kuwa picha hizo ni halali.
Site yetu haijaweza kuthibitisha uhalali ya picha hizo kikamilifu lakini iwapo ni za kweli mauaji hayo yatakuwa mojawapo ya matukio mabaya zaidi kuwahi kuikumba Iraq tangu majeshi ya Marekani kuingia nchini humo mwaka 2003.

Awali video iliyorekodiwa ilionyesha mamia ya watu wakilazimishwa kuelekea katika kityuo kimoja huku sauti ikieleza kuwa ni wanajeshi waliokubali kushindwa.
Duru kutoka vuguvugu la waasi zinasema idadi kubwa ya watu waliotekwa wameuawa.
Mji wa Tikrit ulitekwa na waasi Jumatano wiki iliyopita na majeshi ya Iraq yalikubali kushindwa bila pingamizi.


Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

  • Matamshi kuhusu ubakaji yakera India Matamshi ya mwanasiasa mmoja mwanamke nchini India kuhusu ubakaji yamelaaniwa na watu wengi kote nchini humo. Asha Mirge, ambaye ni mwanachama wa kikundi… Read More
  • Meli yalipuka Bandarini huko Japan...    Mlipuko mkubwa umetokea kwenye meli kubwa ya mafuta nchini Japan katika Pwani ya Kusini Magharibi mwa bandari ya Himeji na kusababisha mtu mmoja kati ya wanane waliokuwa ndani ya meli hiyo kupotea huku wengi… Read More
  • Kumbe mhadhiri UDSM ndio Rais mpya wa Malawi Kwa ushindi wa Profesa Mutharika katika kiti cha urais wa Malawi, anaongeza idadi ya jamii ya wasomi waliopitia Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), ama wakiwa wahadhiri au wanafunzi, kwani alifundisha chuoni … Read More
  • Serikali yamtuhumu Balozi wa Uingereza  Serikali imetangaza rasmi mgogoro wa kidiplomasia kati yake na Balozi wa Uingereza nchini ikimtaka kujieleza kwa madai ya kuingilia mambo ya ndani ya nchi. Mgogoro huo ulitangazwa bungeni mjini Dodoma jana… Read More
  • Mutharika rais mpya nchini Malawi   Mgombea wa Chama cha upinzani nchini Malawi Peter Mutharika ametangazwa mshindi katika uchaguzi wa urais uliozua utata. Mutharika wa Chama cha Democratic Progressive Party amepata asilimia 36.4 ya kura, imetangaz… Read More

0 comments:

Post a Comment