Facebook

Tuesday, 17 June 2014

Saudi Arabia yakataza vibarua kufanya kazi juani

 
 
 
 
 
 
Sheria mpya za kazi zimeanzishwa nchini Saudi Arabia kwa watu wanaofanya kazi nje, kwenye jua.
Kutoka sasa hadi September, vibarua hawaruhusiwi kufanya kazi nje kutoka saa 6 mchana hadi 9 jioni, kwa sababu ya masilahi ya afya yao.
Wafanyakazi kwenye mitambo ya mafuta na kazi za lazima za ukarabati, hawahusishwi na uamuzi huo ikiwa hatua zinachukuliwa kuwakinga na jua.
Nchi jirani ya Qatar, imelaumiwa sana kwa kuwalazimisha vibarua kutoka India kufanya kazi kutwa nje, wakijenga mwahala mwa mashindano ya kandanda ya mwaka wa 2022.
Imesema itachukua hatua kufanya mazingira yao ya kazi kuwa bora.
 
 
Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

0 comments:

Post a Comment