Monday, 19 May 2014
Kashfa nzito Bajeti ya Nishati na Madini
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono wameingia katika mvutano baada ya ujumbe wa maandishi wa kutaka kukwamisha bajeti ya wizara hiyo kusambazwa kwa wabunge.
Habari za uhakika zilizopatikana jana zilieleza kuwa kiini cha mgogoro huo ni ujumbe mfupi (SMS) ambao unamtuhumu Mkono kula njama za kutaka kukwamisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini.
Chanzo hicho limedokezwa kuwa, SMS hiyo inadaiwa kutumwa na Waziri Muhongo kwenda kwa baadhi ya wabunge akimtuhumu Mkono kuwahonga baadhi ya wabunge Sh3 milioni kila mmoja ili kukwamisha bajeti hiyo.
Ujumbe huo unasomeka ”Mhe Spika wa Bunge la Jamhuri, Sisi wabunge waadilifu tunakiri kwamba Mhe Mkono ametufuata na kutupatia fedha kila mmoja milioni 3 ili tukwamishe bajeti ya Nishati na Madini.
Ujumbe huo umeanza pia kusambaa kwenye mitandao ya kijamii ikiwamo Jamii Forums .
Mkono
Mkono ambaye pia ni Mwanasheria mashuhuri nchini, alipoulizwa jana kama ni kweli amelalamika kwa Spika juu ya jambo hilo, alikiri na kusema alichofanya ni kulalamika kwa Spika na amemwachia alishughulikie.
“Ni kweli nimelalamika kwa Spika. Unajua taratibu za Bunge ni kuna any complaint (lalamiko) unaliwasilisha officially (rasmi) kwa Spika… hilo jambo lipo nimelifikisha kwa Spika wao ndiyo watafuatilia kwa taratibu zao,”alisema.
Profesa Muhongo
Alipotafutwa kwa njia ya simu ili alitolee ufafanuzi suala hilo, Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo alituma ujumbe kwa simu ukisema:
“Tutavuka tukiwa na ushindi wa maskini na wanyonge wa nchini mwetu. Tutaendelea kujenga uchumi imara utakaotoa ajira mpya na matumaini mapya kwa vijana, maskini na wanyonge wa nchini mwetu. Watanzania wamechoshwa na wizi, udalali, ubabaishaji na rushwa.”
Mkurugenzi wa shughuli za Bunge, John Joel alipotafutwa jana alisema yeye hana taarifa juu ya jambo hilo akisema kama lipo, basi huenda likawa mikononi mwa Spika mwenyewe
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com uweze kujua kitakachojiri kuhusiana na kashfa hii ndani ya Wizara ya Nishati na Madini
Related Posts:
Matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu Tanzania 2015 kubandikwa katika vituo vya kupigia Kura.Katika kila kituo cha kupigia kura yatabandikwa matokeo ya Diwani, Mbunge pamoja na Rais, amesema Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi Jaji Damian Lubuva. Hivyo katika kila kituo wananchi wa eneo hilo watajua Rais, Mbunge na Diwan… Read More
Mapokezi ya Dr.Magufuli katika Mji wa Chato.5Tutakuwa tunakuletea picha za matukio yote katika kila kitakachokuwa kinaendelea.Kupitia hapa. Unachotakiwa kufanya ni kuingia katika link hii mara kwa mara uweze kujionea kila kitakachokuwa kinajiri. Saa 11:50 JIONI Jioni h… Read More
ACT WAZALENDO wahitimisha siku 10 tangia waanze Kampeni.Mgombea ubunge wa Jimbo la Kijitoupele kupitia Chama Cha ACT-Wazalendo, Zaitun Ali Khamis akihutubia mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Kwamabata mkoani Mjini Magharibi, Zanzibar jana. Picha na Anthony Siame Dar es Salaam. C… Read More
Mh.Lowassa aanza kampeni mkoa wa Kagera,aahidi neema kwa wakulima.Mh.Lowassa hapo jana alianza ziara mkoa wa Kagera kwa kishindo na kuahidi neema kwa wakulima. Mgombea urais wa UKAWA Mh Edward Lowassa ameingia kwa kishindo katika mkoa wa Kagera na amesema akichaguliwa kuwa rais mikoa yenye … Read More
Mgawanyo wa Majimbo wamtingisha James Mbatia Vunjo.Moshi. Wagombea udiwani wa Chadema katika kata 16 za Jimbo la Vunjo lililopo mkoani Kilimanjaro, wametangaza kutomuunga mkono mgombea ubunge wa jimbo hilo wa NCCR Mageuzi ambacho ni kati ya vyama vinavyounda Umoja wa Katiba y… Read More
0 comments:
Post a Comment