Takriban watu 27 wakiwemo watoto na wanawake wameuawa katika mapigano Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo.
Yanaaminika kuwa mapigano ya kikabila. Waathiriwa wote walikuwa watu wa kabila la Bafuliru.
Haijulikani nani aliyetekeleza mashambulizi hayo lakini eneo hilo limeshuhudia mgogoro kati ya watu wa kabila la Bafuliru na Barundi
Mwandishi wa shirika la habari la Reuters alisema kuwa waathiriwa walipigwa risasi , kudungwa visu au kuchomwa wakiwa ndani ya nyumba zao.
Waziri wa mambo ya ndani wa jimbo la Kivu Kusini, Jean-Julien Miruho aliambia shirika la habari la Agence France Presse kuwa uvamizi huo ulikuwa uvamizi wa kulipiza kisasi kwa wizi wa mifugo.
Tuko katika maboresho hivi karibuni
blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za
kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano
mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia
kupitia www.bantutz.com....
0 comments:
Post a Comment