Facebook

Thursday, 5 June 2014

Kuelekea Michuano ya Kombe la dunia,Polisi waongezwa mishahara Brazil

Polisi waliandamana wakitaka nyongeza ya mishahara
Serikali ya Brazil inapendekeza kuwapa nyongeza ya asilimia 15.8 mishahara polisi wake ili wasigome wakati wa ufunguzi wa michuano ya kombe la dunia wiki ijayo.
Maafisa wakuu wa polisi watapokea nyongeza ya asilimia 12 kuanzia mwezi Julai na nyingine ya asilimia 3.8 mwezi Januari.
Makubaliano hayo yanakuja baada ya mgomo wa polisi mapema mwaka huu ambapo takriban watu 250,000 walishiriki.
Maandalizi ya kombe la dunia ambalo linaanza tarehe 12 Juni, yamekumbwa na maandamano ya kupinga serikali kwa kutumia gharama kubwa kuandaa michuano hiyo.
Polisi ambao hukabiliana na vitendo vya uhalifu na kupambana na ulanguzi wa madawa ya kulevya pamoja na ugaidi, pia watahakikisha usalama mipakani na katika viwanja vya ndege.
'Mgomo wasitishwa'
Maandamano ya polisi mjini Rio
Chama cha wafanyakazi kinachowawakilisha maafisa hao wa polisi, Fenapef, kimeelezea kufurahishwa na hatua ya serikali kuwaongea mishahara kabla ya kuanza kwa michuano ya kombe la dunia na kabla ya uchaguzi tarehe 5 Oktoba.
Mkuu wa chama hicho alisema kuwa serikali pia imekubali kubuni kikundi cha waakilishi watakaozungumzia swala la kuwapandishwa vyeo polisi waliofika kiwango hicho.
Mwezi jana polisi hao waligoma wakitaka kuongezwa mishahara katika majimbo 14 nchini humo huku walimu na wafanyakazi wa umma pia wakidai mazingira bora ya kazi na nyongeza ya mishahara.
Serikali imeimarisha usalama katika maeneo yote 12 yatakayotumiwa kwa michuano hiyo huku polisi 20,000 wakitarajiwa kudhbiti ulinzi mjini Rio.
Wadadisi wanasema kuwa hatua ya serikali ni kutaka kuhakikisha kuwa maandamano yaliyoshuhudiwa wakati wa kombe la mashirikisho mwaka jana hayatashuhudiwa tena.



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari,tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.

Related Posts:

  • Binti alazimisha penzi kwa kumshikia Bastola mwanaume.Marekani: Binti (25) akamatwa kwa kosa la kumlazimisha kijana (33) kufanya naye mapenzi akiwa kamshikia bastoka kwenye gari lake baada ya kijana huyo kuomba lift. Inasemekana huyo binti alikuwa na mwanamke mwingine ambaye wal… Read More
  • Nyama ya Kiboko yawaletea maafa Afrika KusiniWatu kumi walikanyagwa na gari lililokuwa linakwenda kwa mwendo wa kasi walipokuwa wanajaribu kujipatia angalau kipande cha nyama ya Kiboko mwishoni mwa wiki. Taarifa hii ni kwa mujibu wa mtandao wa Daily Nation. Kiboko huyo … Read More
  • Tahadhari kuhusu gesi za sumuMkuu wa shirika la utabiri wa hali ya anga la Umoja wa Mataifa Michel Jarraud, ametoa tahadharti kuwa dunia nzima inapaswa kushughulikia mabadiliko ya hali ya anga haraka iwezekanavyo la sivyo muda unakwisha. Takwimu mpya kut… Read More
  • Miaka 8 jela kwa jaribio la kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa RwandaWatu wanne - Watanzania wawili na Wanyarwanda wawili- waliokutwa na hatia ya kutaka kumuua mkosoaji wa Rais wa Rwanda Paul Kagame nchini Afrika Kusini wamehukumiwa kwenda jela kwa miaka minane kila mmoja. Mkuu wa zamani wa je… Read More
  • Mahakama:Pistorius hakukusudia kuuaJaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji inayomkabili Oscar Pistorius, amesema upande wa mashitaka umekosa kuthibitishia kikamilifu shitaka kuu la kwanza dhidi ya Pistorius kuwa alikusudia kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp… Read More

0 comments:

Post a Comment