Facebook

Wednesday, 11 June 2014

Mhubiri mwingine auawa nchini Kenya


Marehemu Sheikh Mohammed Idris ameuawa na watu wasiojulikana
Muhubiri wa kiisilamu ameuawa mjini mombasa pwani ya Kenya , ikiwa ni mauaji ya hivi karibuni ya kiongozi mwingine wa kidini.
Sheikh Mohammed Idris, ambaye ni mwenyekiti wa baraza la maimamu na wahubiri nchini Kenya, aliuawa karibu na msikiti ulio karibu na nyumba yake na watu wasiojulikana.
Duru zinasema kwa alikuwa amepokea vitisho kutoka kwa vijana wenye itikadi kali za kidini na tayari alikuwa ameelezea hofu juu ya maisha yake.
Wahubiri kadhaa mashuhuri wameuawa katika hali ya kutatanisha katika miaka ya hivi karibuni.
Wengine waliuawa kwa madai ya kuwa na uhusiano wa karibu na kundi la wanamgambo la al-Shabaab huku wafuasi wao wakiilaumu serikali kwa mauaji yao, madai ambayo serikali imakenusha.
Marahemu Idris alikuwa ameitaka serikali kukabiliana na baadhi ya watu wenye itikadi kali za kidini ndani ya msikiti hali ambayo ilisababisha baadhi ya waumini kumuita msaliti.



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

Related Posts:

  • Kiongozi ataka vijana wajihami Nigeria Wapiganaji wa Boko Haram wamekuwa wakiwahangaisha wananchi kwa miaka mingi Kiongozi mmoja wa kijamii katika mji wa Chibok Nchini Nigeria ameiomba serikali ya taifa hilo kuwaruhusu kubuni makundi ya vijana waliojiham… Read More
  • Mashoga wapinga Urais wa Kutesa UN Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uganda, Sam Kutesa. Uwezekano wa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Uganda, Sam Kutesa, kushinda cheo cha Urais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kumeanzisha mjadala mkali nchini Uganda,… Read More
  • Majeshi ya DRC na Rwanda yakabiliana Majeshi ya DRC yakabili wanajeshi wa Rwanda mashariki mwa Congo Maafisa wakuu katika Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo wanasema kuwa makabiliano makali ya… Read More
  • Kutana na kisa hiki cha kahaba wazee wa Korea Kusini Wazee katika baadhi ya nchi huheshimika na kuwa akiba ya busara kwa kizazi cha vijana na zaidi ya yote huangaliwa na kusaidiwa kimaisha. Huko nchini Korea Kusini maisha kwa wazee ambao walichangia katika uchumi wa t… Read More
  • Wadau wakutana kupinga ubakaji vitani Angelina Jolie ni mmoja wa wanaharakati maarufu wanaopinga dhuluma za kingono ikiwemo ubakaji Viongozi wa kimataifa wanakutana jijini London kwa wiki nzi… Read More

0 comments:

Post a Comment