Marehemu Sheikh Mohammed Idris ameuawa na watu wasiojulikana
Muhubiri wa kiisilamu ameuawa mjini mombasa pwani ya Kenya , ikiwa ni mauaji ya hivi karibuni ya kiongozi mwingine wa kidini.
Sheikh Mohammed Idris, ambaye ni mwenyekiti wa
baraza la maimamu na wahubiri nchini Kenya, aliuawa karibu na msikiti
ulio karibu na nyumba yake na watu wasiojulikana.Wahubiri kadhaa mashuhuri wameuawa katika hali ya kutatanisha katika miaka ya hivi karibuni.
Wengine waliuawa kwa madai ya kuwa na uhusiano wa karibu na kundi la wanamgambo la al-Shabaab huku wafuasi wao wakiilaumu serikali kwa mauaji yao, madai ambayo serikali imakenusha.
Marahemu Idris alikuwa ameitaka serikali kukabiliana na baadhi ya watu wenye itikadi kali za kidini ndani ya msikiti hali ambayo ilisababisha baadhi ya waumini kumuita msaliti.
Tuko katika maboresho hivi karibuni
blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za
kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano
mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia
kupitia www.bantutz.com....
0 comments:
Post a Comment