Facebook

Tuesday, 10 June 2014

Nando afunguka kuhusu stori zilizo sambaa kuwa ana mahusiano ya kimapenzi na Lulu Michael

Mshiriki wa shindano la Big Brother Africa (the chase) 2013, Amir Nando ameweka wazi kuwa hajawai kuwa na uhusiano ya kimapenzi na mwanadada wa filamu, Elizabeth Micheal aka Lulu, lakini anakubali sana.

Nando amezungumzia pia mipango yake ya kufanya filamu na mwanadada huyo wa filamu.

“Lulu nishaonana nae, mara mbili mara tatu lakini sina uhusiano nae na sijawai kuwa na uhusiano nae, ila namkubali sana, mwanamke unajua mzuri, shepu, mwonekano wake, michezo yake, tunaonana tu ile oya niaje mara mbili mara tatu. Na proposal mimi, akitaka tukae chini tutengeneze movie, hicho ndicho nachotaka nifanye, akikubali tutafanya, lakini Lulu ni mkali, niko tayari kumuoa lakini sijamwambia, Kwa sasa ni mshikaji wangu tu na napenda kazi zake. Huwa ni mtu ambaye napenda kufuatilia ishu zake” Alisema Nando.
 
 
Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment