Nana Kwaku Bonsam, amesema yeye ndiye anayemroga nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno, ili asicheze mchezo wa kundi la saba katika fainali za kombe la dunia ambapo timu ya taifa ya Ureno itapambana na timu ya taifa ya Ghana, Black Stars.
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ureno Paul Bento alisema pamoja na kutarajia kumkosa Ronaldo katika mchezo wa juzi wa kirafiki, bado hajafahamu ni lini mshambuliaji huyo atakuwa fit kwa ajili ya kujiunga na wenzake.
Mshambuliaji huyo wa klabu ya Real Madrid anasumbuliwa na maumivu ya mishipa fulani laini katika mguu wake, ambapo kwa mara ya mwisho alionekana uwanjani wakati wa mchezo wa hatua ya fainali ya ligi ya mabingwa barani Ulaya walipocheza dhidi ya Atletico Madrid.
Tuko katika maboresho hivi karibuni
blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za
kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano
mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia
kupitia www.bantutz.com....

0 comments:
Post a Comment