Facebook

Tuesday, 10 June 2014

7 wakamatwa kwa dhuluma ya ngono Misri

Wiki jana Misri ilifanya dhuluma za kingono kuwa uhalifu ambao adhabu yake ni miaka 5 jela
Wanaume saba wamekamatwa nchini Misri, baada ya kushukiwa kuwadhulumu kiongono wanawake katika sherehe za Jumamosi za kumkabidhi rasmi mamlaka Rais Abdul Fattah al Sisi.
Hatua ya kuwakamata wanaume hao, inakuja baada ya kanda ya video kusambazwa kwenye internet ikionyesha mwanamke akivuliwa nguo na kuvamiwa na genge la wanaume
Haijulikani ikiwa kanda hiyo ilinaswa, lakini walioshuhudia kitendo hicho alisema kwambwa unyama huo ulitokea Jumapili usiku.
Wiki jana maafisa wa utawala nchini Misri, waliharamisha dhuluma za kingono na kuufanya uhalifu kwa mara ya kwanza adhabu yake ikiwa miaka mitano jela kwa watakaopatikana na hatia.



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

 

0 comments:

Post a Comment