Facebook

Tuesday, 10 June 2014

7 wakamatwa kwa dhuluma ya ngono Misri

Wiki jana Misri ilifanya dhuluma za kingono kuwa uhalifu ambao adhabu yake ni miaka 5 jela
Wanaume saba wamekamatwa nchini Misri, baada ya kushukiwa kuwadhulumu kiongono wanawake katika sherehe za Jumamosi za kumkabidhi rasmi mamlaka Rais Abdul Fattah al Sisi.
Hatua ya kuwakamata wanaume hao, inakuja baada ya kanda ya video kusambazwa kwenye internet ikionyesha mwanamke akivuliwa nguo na kuvamiwa na genge la wanaume
Haijulikani ikiwa kanda hiyo ilinaswa, lakini walioshuhudia kitendo hicho alisema kwambwa unyama huo ulitokea Jumapili usiku.
Wiki jana maafisa wa utawala nchini Misri, waliharamisha dhuluma za kingono na kuufanya uhalifu kwa mara ya kwanza adhabu yake ikiwa miaka mitano jela kwa watakaopatikana na hatia.



Tuko katika maboresho hivi karibuni blog hii itakuwa ni site ambayo itaitwa www.bantutz.com ni katika hatua za kuboresha huduma zetu za kutoa habari na burudani.Tutakuja katika muonekano mpya na bora zaidi.Vitu vizuri vipya usivyotarajia utaviona na kufurahia kupitia www.bantutz.com....

 

Related Posts:

  • Wafanyakazi wambaka binti mwenye miaka 6 India.   Polisi katika mji wa Bangalore, kusini mwa India wanasema wafanyakazi wawili wa shule moja wanatuhumiwa kumbaka binti mwenye umri wa miaka sita. Mtoto huyo alifanyiwa kitendo hicho Julai 2, lakini wazazi wake wa… Read More
  • TUFANI LAZUA TAFRANI UFILIPINO   Upepo mkali umesababisha umeme kukatika na kulazimisha maelfu ya watu kukimbia makazi yao kufuatia Tufani Rammasun kugonga visiwa vya Ufilipino. Tufani hilo ambalo pia linajulikana kama Glenda, liligonga kisiw… Read More
  • Serikali na Waasi wabadilishana wafungwa Mali.   Serikali ya Mali na waasi wa Tuareg wamebadilishana wafungwa kama ishara ya wema kabla ya kuanza mazungumzo ya amani. Jeshi limesema wanajeshi 45 waliokuwa wakishikiliwa na waasi kaskazini mwa nchi hiyo waliwasil… Read More
  • ISRAEL KUENDELEA NA MASHAMBULIZI GAZA   Israel imeonya maelfu ya Wapalestina mashariki na kaskazini mwa Gaza na kuwataka kuondoka majumbani mwao huku ikiendelea na mashambulizi ya anga. Onyo hilo linakuja baada ya mpango wa kusitisha mapigano wa Mi… Read More
  • Moto wateketeza karatasi za kura Malawi.    Zaidi ya karatasi elfu moja za kura za uchaguzi uliokuwa na utata wa Malawi, zimeteketezwa na moto katika mazingira ya kutatanisha. Chama cha upinzani cha MCP kilitaka kura hizo zihesabiwe upya za kiti ch… Read More

0 comments:

Post a Comment