Facebook

Tuesday, 17 June 2014

Gwiji Michael Schumacher atoka kwenye 'coma'

Michael Schumacher alikuwa akitibiwa kwenye hospitali ya Chuo Kikuu cha Grenoble nchini Ufaransa.
Michael Schumacher alikuwa akitibiwa kwenye hospitali ya Chuo Kikuu cha Grenoble nchini Ufaransa.
Bingwa wa Formula 1 Michael Schumacher ameondoka hospitali mjini Grenoble na hayupo tena kwenye coma, imeeleza familia yake.

Raia huyo wa Ujerumani, 45, ataendelea na matibabu kwenye eneo ambalo halijatajwa, familia yake ilieleza kwenye taarifa.
Schumacher aliwekwa kwenye hospitali ya magonjwa ya coma baada ya kupata majeraha makali kichwani aliyoyapata kwenye ajali ya mcezo wa kuteleza barafuni katika vilima vya Ufaransa Desemba 29.
Familia yake imewashukuru watu waliotuma ujumbe wa kumuunga mkono, wanasema: “Tuna uhakika ilimsaidia sana”.
Pia walisifia kazi nzuri ya madaktari wa hospitali ya Grenoble, kusini-mashariki mwa Ufaransa.
Madaktari walimuweka bingwa huyo mara saba wa mbio za magari kwenye coma kupunguza kuvimba kwa ubongo wake.

Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

0 comments:

Post a Comment