Facebook

Sunday, 1 June 2014

Kolo Toure augua malaria,ashindwa kucheza mechi...

Photo: KOLO TOURE APATA MALARIA
Beki wa Liverpool na Ivory Coast Kolo Toure amepata malaria, na kushindwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Bosnia-Herzegovina.  
Toure aliugua wakati akisafiri kwenda Marekani, lakini anatazamiwa kuwa atapona na kuwa tayari kabla ya Kombe la Dunia kuanza.
"Hakushiriki mchezo dhidi ya Bosnia lakini atarejea mapema wiki ijayo," amesema mkuu wa madaktari wa timu, profesa Cyrille Dah.
Yaya Toure pia aliukosa mchezo huo kutokana na tatizo la misuli.
Ivory Coast wapo kundi C pamoja na Columbia, Ugiriki na Japan.

Beki wa Liverpool na Ivory Coast Kolo Toure amepata malaria, na kushindwa kucheza mechi ya kirafiki dhidi ya Bosnia-Herzegovina.
Toure aliugua wakati akisafiri kwenda Marekani, lakini anatazamiwa kuwa atapona na kuwa tayari kabla ya Kombe la Dunia kuanza.
"Hakushiriki mchezo dhidi ya Bosnia lakini atarejea mapema wiki ijayo," amesema mkuu wa madaktari wa timu, profesa Cyrille Dah.
Yaya Toure pia aliukosa mchezo huo kutokana na tatizo la misuli.
Ivory Coast wapo kundi C pamoja na Columbia, Ugiriki na Japan.
 
Endelea kutembelea katemimethsela.blogspot.com kupata taarifa mbalimbali za kimichezo na burudani

Related Posts:

  • Ghana yakana kupanga mechi Brazil Rais wa shirikisho la soka nchini Ghana , amekanusha madai kuwa shrikisho hilo lilikubali timu ya Taifa kucheza katika mechi ambazo tim… Read More
  • Van Gaal: ''FIFA imetuonea'' Van Gaal akashifu FIFA kwa ratiba mbaya za mkondo wa pili Kocha wa Uholanzi Louis van Gaal amelishutumu shirikisho la soka duniani FIFA kwa "kufanya hila" kwa jinsi linavyopanga ratiba ya michuano ya Kombe la Dunia… Read More
  • Uholanzi kumenyana na Mexico Uholanzi kuvaana na Mexico mkondo wa pili Uholanzi ilimaliza katika nafasi ya kwanza kwenye kundi B kufuatia ushindi wa mabao 2-0 katika mechi yao ya mwisho ya makundi. Mabao ya Uholanzi yaliyofungwa na Leroy Fern na… Read More
  • Algeria yailaza Korea Kusini 4-2 Algeria ambayo ilikuwa imeshindwa 2-1 na Ubeljiji katika mechi yao ya ufunguzi katika kundi H iliingia katika mechi hii ikifahamu fika endapo itashindwa basi haitakuwa na budi kuweka tayari mipango ya kurejea nyum… Read More
  • Origi aisaidia Ubeligiji kusonga mbele   Kinda aliyezaliwa Kenya na kuchukua uraiya wa Ubeligiji Divock Origi alifungia Ubeligiji bao la pekee na la ushindi dhidi ya Urusi katika mechi yao ya pili ya kundi H. Bao hilo la dakika za mejeruhi za mechi… Read More

0 comments:

Post a Comment