Facebook

Monday, 9 June 2014

Mabaharia wa meli ya Malaysia waachiliwa


Mabaharia 11 wa meli moja ya Malaysia iliotekwa nyara na maharamia wa Somali wameachiliwa huru baada ya kuwa mateka kwa takriban miaka mitatu.
Mabaharia hao kutoka Kusini mwa bara Asia na Iran walikuwa wameabiri meli hiyo ya makasha MV Albedo wakati ilipotekwa nyara yapata kilomita 1500 kutoka pwani ya Somali.
Maelezo kuhusu vile walivyoachiliwa bado hayajatolewa,lakini afisa mmoja wa Umoja wa Mataifa Nick Kay amesema kuwa wanasafirishwa hadi nchini Kenya kabla ya kurudishwa makwao.
Mabaharia saba wa meli hiyo waliwachiliwa miaka miwili iliopita baada ya kikombozi kulipwa.
Sita wengine wamefariki mmoja akipigwa risasi huku wengine wakifa maji baada ya kimbunga kikali kupiga meli hiyo mwaka uliopita.
Umoja wa mataifa unakadiria kwamba takriban watu 40 bado wanazuiliwa na maharamia wa kisomali .

Related Posts:

  • Juhudi za kutafuta amani Gaza zaingia dosari. Wapalestina zaidi ya 800 wameuawa na Waisraeli 35 Israeli imeendelea kuivirumishia makombora Gaza kucha kutwa ,huku kikao cha mawaziri wa baraza la Usalama kikitarajiwa huko Marekani kujadili mapendekezo mapya ya … Read More
  • Sudan kusini yakabiliwa na baa la njaa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita ku… Read More
  • Gaza:Makubaliano ya saa 12 yaheshimiwa Kiongozi wa Hamas na mwenzake wa Israel Serikali ya Israel na wapiganaji wa Hamas wameanza kutekeleza makubaliano ya kusitisha vita kwa masaa 12 katika … Read More
  • Sudan kusini yakabiliwa na baa la njaa Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita ku… Read More
  • Maandamano yazuka Palestina polisi wakabiliana na raia Palestina Maandamano makubwa yamefanyika katika ukingo wa Magharibi mwa Palestina karibu na mpaka wake na Israel kupinga mashambulio yanayofanywa na Israel. Waandamanaji hao wakiwa na hasi… Read More

0 comments:

Post a Comment