Facebook

Sunday, 15 June 2014

Maradona:"TIKI-TAKA" imefeli,Mourinho alikuwa sahihi kumtema Casillas.


Diego Maradona
LEJENDARI wa Argentina, Diego Armando Marando, amewaponda Mabingwa wa Dunia Spain kwa kushindwa kusoma alama za nyakati na sasa ‘tiki-taka’ imekufa baada kufumuliwa Bao 5-1 na Netherlands Juzi kwenye Mechi ya Kundi B la Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Vile vile, Maradona amemlaumu Kipa wa Spain Iker Casillas kwa kufungisha Bao 2 na kusema hilo linaonyesha Jose Mourinho hakufanya makosa alipomtema Kipa hiyo wakati akiwa Meneja wa Real Madrid.
Juzi, Spain walibomolewa Bao 5-1 na Netherlands licha ya wao kutangulia mbele kwa Bao 1 la Penati ya Xabi Alonso lakini Netherlands wakaja juu na kushindilia Bao 5 kupitia Arjen Robben na Robin van Persie, waliofunga Bao 2 kila mmoja, na Stefan De Vrij kufunga 1.
Maradona anaamini Kikosi cha Kocha Vicente del Bosque kimeshindwa kuchukulia kwa uzito onyo kutoka Barcelona ambao Msimu huu walizorota mno na kutoka kapa bila Taji kubwa lolote.
Maradona, mwenye Miaka 53, amenena: “Timu ya Spain imezidi kuzeeka na hilo lilidhihirika walipocheza na Netherlands. Spain wamekuwa wakicheza tiki-taka kwa muda sasa. Ni njia njema kucheza Soka na Dunia nzima imefurahia. Iliwafanya washinde Mataji matatu makubwa mfululizo kuanzia 2008 hadi 2012. Lakini Vicente del Bosque angekumbuka Klabu huko Ulaya zishapata jibu la staili ya Barca ambayo ni hiyo hiyo wanayocheza Timu ya Taifa ya Spain. Mchezo wa haraka wa mashambulizi ya kaunta-ataki yamewazidi maarifa sasa! Lakini Spain imegoma kubadilika licha ya wapinzani kugundua dawa yake! ”
Kipigo hicho cha Spain cha 5-1 ndicho kikubwa kwa Bingwa Mtetezi wa Kombe la Dunia katika Mechi ya Kwanza na hicho kilikuwa kipigo chao cha pili katika Mechi zao 55.
Maradona aliwasifia mno Robin van Persie na Arjen Robben na kumlaumu Kipa Iker Casillas kwamba hakucheza vizuri.

MARADONA: ‘MOURINHO NI SAHIHI KUHUSU CASILLAS!!’
Diego Maradona amesema uchezaji mbovu wa Kipa Iker Casillas umedhihirisha Jose Mourinho hakukosea kumtema wakati alipokuwa Meneja wa Real Madrid.
Mwenyewe Casillas amekubali kwamba anapaswa kulaumiwa kwa kipigo hiki toka kwa Netherlands na Maradona ameeleza: “Alikuwa na Gemu mbovu ambayo sijaona maishani..inanikumbusha nini Rafiki yangu Mourinho alikuwa akiwaeleza Watu!”
Aliongeza: “Alisema Casillas hakuwa Kipa sahihi lakini badala yake hilo lilimfanya aondolewe Real!”

Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

  • VAN GAAL :MOURINHO AMEJIJENGA MWENYEWE Meneja wa Manchester United Louis van Gaal amesisitiza kuwa hajafanya lolote kubwa kusababisha Jose Mourinho kuwa moja ya makocha wenye mafanikio duniani. Mourinho, ambaye ni meneja wa Chelsea kwa sasa, alifanya kazi chini y… Read More
  • Tanzania yaifumua Benin 4-1Taifa Stars imeitungua Benin kwa mabao 4-1 katika mechi ya kitarafiki ya kimataifa iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Mabao ya Stars yalifungwa na wachezaji wake wawili wanaokipiga nchini na wawili w… Read More
  • Majeruhi wazidi kuongezeka Arsenal.   Kwa sasa tuna wachezaji kumi wa kikosi cha kwanza wapo nje kwa majeruhi. Katika mchezo wa jana wa timu ya taifa Uingereza kufuzu Euro 2016 Danny Welbeck alitonesha enka yake na kutolewa nje dakika 10 kabla ya mpi… Read More
  • Diego Costa hatihati. Diego Costa huenda akacheza katika mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Manchester United licha ya kuugua na kulazimika kupelekwa hospitali. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Spain, 26, amekuwa akipata nafuu akiwa nyumbani na … Read More
  • Manchester United yabanwa mbavu Ligi Kuu Uingereza.   Ligi kuu ya England imeendelea jana usiku ambapo Manchester United ilijikuta ikibanwa mbavu na kushindwa kufurukuta ugenini kwa West Bromwich Albion na kutoka sare ya mabao 2-2 licha kwamba ilitawala mc… Read More

0 comments:

Post a Comment