Facebook

Monday, 16 June 2014

Penny afunguka baada ya kupona.


MTANGAZAJI wa maarufu wa runinga Bongo, Peniel Mungilwa ‘Penny’ amefunguka kuwa ugonjwa uliompiga juzikati ulikuwa ‘serious’ kiasi cha kuona ni Mungu tu amemwokoa.

Akichezesha taya na paparazi wetu, Penny alisema anamshukuru Mungu anaendelea vizuri kwani alikuwa na hali mbaya baada ya kubanwa na ugonjwa wa Athma kwa siku tatu nzima akiwa anasaidiwa kupumua na mashine ya oxygen.

“Ukweli nilikuwa na hali mbaya huwa nasumbuliwa na Athma mara kwa mara lakini naweza kubanwa kwa siku moja ila ya safari hii imekuja kwa nguvu sana kwa sababu ilikuja na mafua makali jambo lililosababisha nilazwe kwa siku tatu katika Hospitali ya  AAR huku nikipumua kwa kutumia mashine, kweli Mungu ni mkubwa, ninaendelea vizuri,”

Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com
 

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment