Facebook

Tuesday, 19 August 2014

Dunga ateua kikosi kipya cha Brazil;Wapya kibao wajumuishwa

Baada ya kuteuliwa kwa mara ya pili kuinoa timu ya taifa ya Brazil "SELECAO".

Dunga,ameteua kikosi cha wachezaji 22 kitakachovaana na Colombia huko Miami nchini Marekano mnamo September 5 mwaka huu.

Na baada ya hapo siku nne baadae itavaana na Ecuador huko New Jersey katika Gillette Brasil Global Tour

Katika kikosi hicho Dunga amewajimuisha wachezaji mbalimbali ambao hawakuitwa katika kikosi kilichoshirili fainali za Kombe la dunia.

Dunga amewajumuisha wachezaji wawili mahiri kutoka Fc Porto ya nchini Ureno;Danilo na Alex Sandro.

Vilevile kamuita Rafael Cabral kutoka klabu ya Napoli na kiungo wa Corinthians Elias.

Nyota wawili kutoka Cruzeiro  Ricardo Goulart na Everton
Ribeiro wameitwa kwa mara ya kwanza timu ya taifa baada ya kufanya vizuri katika Ligi kuu ya nchini Brazil "Brasileirao" msimu uliopita na kufanikiwa kunyakua Ubingwa wa Ligi hiyo.

Nyota wa Liverpool Philippe Coutinho na mchezaji mpya aliyesajiliwa na Chelsea Filipe Luis pia ni baadhi ya wachezaji walioitwa na Dunga kwa mara ya kwanza timu ya taifa Brazil alipoteuliwa kuwanoa Selecao .

Dunga ameongeza wachezaji wapya 10 kati ya 23 walionyanyaswa vibaya na Ujeruman katika nusu fainali waliyofungwa magoli 7-0 mwezi uliopita.

KIKOSI KAMILI

>MAGOLIKIPA
Jefferson (Botafogo)
Rafael Cabral (Napoli)

MABEKI
David Luiz (Paris Saint-Germain)
Marquinhos (Paris Saint-Germain)
Gil (Corinthians)
Miranda (Atletico Madrid)
Maicon (Roma)
Filipe Luis (Chelsea)
Alex Sandro (FC Porto)
Danilo (FC Porto)

VIUNGO
Luiz Gustavo (Wolfsburg)
Elias (Corinthians)
Fernandinho (Manchester City)
Ramires (Chelsea)
Willian (Chelsea)
Everton Ribeiro (Cruzeiro)
Oscar (Chelsea)
Coutinho (Liverpool)

WASHAMBULIAJI
Ricardo Goulart (Cruzeiro)
Hulk (Zenit)
Neymar (Barcelona)
Diego Tardelli (Atletico MG)

Imeandaliwa na........
                              Katemi Methsela
                    
Endelea kutembelea www.bantutz.com uweze kupata habari mbalimbali za michezo kwa muda muafaka.

Related Posts:

  • MATOKEO YAZUA VURUGU ARGENTINA   Polisi wa Argentina wamepambana na waandamanaji katika mji mkuu, Buenos Aires baada ya nchi hiyo kufungwa na Ujerumani katika mchezo wa fainali ya Kombe la Dunia. Mapema jana jioni maelfu ya watu walikusanyika… Read More
  • Adidas watarajia makubwa baada ya kuingia mkataba mnono na Manchester United   1.Klabu; Manchester United Kampuni; Adidas Thamani(mwaka); £75m Miaka 10; £750m 2.Klabu; Real Madrid Kampuni; Adidas Thamani(mwaka); £31m Miaka 8; £248m 3.Klabu; Chelsea Kampuni; Adidas Th… Read More
  • OSCAR "SIJUI CHA KUSEMA" Kiungo mshambuliaji wa Brazil na Chelsea, amesema hajui nini kimewatokea baada ya mfululizo wa matokeo mabaya katika mashindano ya Kombe la Dunia huko nchini kwao. Hata hivyo, alikubali timu yao haikucheza vyema na … Read More
  • ADHABU YA POWELL YAPUNGUZWA    Bingwa wa zamani wa mbio za mita 100 Asafa Powell na Sherone Simpson wote kutoka Jamaica wamepunguziwa adhabu ya kufungiwa, kutoka miezi 18 hadi miezi sita. Uamuzi uliotolewa na mahakama ya usuluhisi wa m… Read More
  • Ujeruman yapokelewa kwa shangwe.   Maelfu ya mashabiki wa soka nchini Ujerumani wamejitokeza mjini Berlin kuwalaki wachezaji wa timu ya taifa walioshinda Kombe la Dunia. Sherehe kubwa zimefanyika katika eneo la Brandenburg Gate, ambapo wacheza… Read More

0 comments:

Post a Comment