Facebook

Sunday, 18 May 2014

Gerardo Martino ajiuzulu Barcelona !!




 
Gerardo Martino ataacha kazi ya Ukocha wa Barcelona mara baada ya Jana kupokonywa Ubingwa wa La Liga baada kutoka Sare 1-1 na Atletico Madrid ambao wameutwaa Ubingwa huo na kuiacha Barca ikitoka mikono mitupu Masimu huu kitu ambacho hakijawahi kutokea tangu 2007/08.
Akizungumza mara baada ya Mechi hiyo ya Jana, Martino alisema: “Nasikitika sana tumeshindwa kutimiza malengo yetu ambayo Klabu hii Siku zote imeyaweka na kutimiza!”
Martino alishika wadhifa huo Mwezi Julai Mwaka Jana na kumbadili Tito Vilanova ambae alijiuzulu baada kuugua.
Kazi yake hapo Barcelona ilikuwa ya kwanza kwa Martino, Raia wa Argentina, nje ya Marekani ya Kusini tangu ashike wadifa wa Ukocha wa Miezi 6 huko Tenerife, Spain.
Akiwa na Barca, Martino alisimamia ushindi wa Mechi 40 kati ya 59 lakini wakapokonywa Ubingwa wa La Liga, kutupwa nje ya UCL kwenye Robo Fainali na kufungwa Fainali ya Copa del Rey na Real Madrid.

Related Posts:

  • Dante atakiwa Man United.Mchezaji wa kimataifa wa Brazil Dante anatakiwa na timu ya Manchester United kwenda Old Trafford msimu huu. Timu ya Manchester ipo tayari kumpa mkataba mchezaji huyo kujiunga na mashetani hao.Lakini mchezaji mwenyewe Dante am… Read More
  • Skrtel akataa kusaini kataba mpya Liverpool.  Beki wa klabu ya Liverpool Martin Skrtel amefichua kuwa bado hajasaini mkataba mpya na klabu hiyo kama ambavyo inaripotiwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini England pamoja na nyumbani kwao huko Slovakia. Skr… Read More
  • Tetesi zote za Usajili barani Ulaya siku ya leo.Winga wa England Raheem Sterling, 20 hana tatizo na uwezekano wa kuhamia Manchester United kutoka Liverpool, ingawa mchezaji huyo ana wasiwasi kuhusu jinsi uhamisho huo utakavyopokelewa, kwa kuzingatia uhasama baina ya timu h… Read More
  • BantuTz MAGAZETINI:Soma kilichoandikwa katika magazeti yote ya leo Jumamosi,Juni 06   MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusomana kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata hab… Read More
  • Everton yamnasa Tom Cleverley.Everton watamsajili Tom Cleverley kwa mkataba wa miaka mitano wakati mkataba wake na Manchester United utakapomalizika Julai 1. Mchezaji huyo wa kimataifa wa England atakuwa mchezaji wa kwanza kusajiliwa msimu huu na meneja R… Read More

0 comments:

Post a Comment