Kampuni ya Apple imezindua saa ya kisasa -
the Apple Watch - ambayo ni bidhaa yake
mpya tangu iPad ya kwanza na tangu kifo cha
mmoja wa waasisi wake Steve Jobs.
Kifaa hicho huendesha programu tumishi
(apps) na pia hufuatilia mienendo ya kiafya
na vilevile huwasiliana na iPhone.
Wakati wapinzani wa Apple tayari wana saa
za mtindo huo, wataalam wanasema Apple
ina historia ya kuchelewa kuleta bidhaa zake
sokoni lakini hubadili kabisa mwelekeo wake.
Apple pia imezindua simu aina mbili ambazo
ni kubwa kuliko za zamani.
iPhone 6 ina skrini yenye ukubwa wa
sentimita 11.9 na iPhone 6 Plus skrini yake
ina ukubwa wa sentimita 14.0, mabadiliko
ambayo wachambuzi wanasema yatazuia
wateja kuhamia simu za Android.
Apple vilevile imetangaza huduma mpya ya
malipo ijulikanayo kama 'Apple Pay' ambayo
mkurugenzi mkuu Tim Cook amesema ana
imani "itachukua nafasi ya pochi".
Wednesday, 10 September 2014
Apple wazindua bidhaa mpya.
Related Posts:
Mtandao wa WhatsApp wafanya mabadiko katika 'magroup' kwa kuongeza idadi na kuanza kulipiwa baada ya mwezi.Habari njema kwa upande mmoja na vilevile ni habari habari mbaya kwa upande wa pili wa shilingi kwa watumiaji wa Mtandao wa kijamii unaozidi kujizolea umaarufu mkubwa hivi sasa ujulikanao kama WhatsApp. Leo hii Mtandao wa Wha… Read More
Huyu ndiye mhitimu bora wa chuo kikuu cha UDSM mwaka 2014Huyu ndiye mhitimu bora wa chuo kikuu cha UDSM mwaka 2014, anaitwa Doreen Kabuche ana miaka (22). Alitangazwa kuwa kinara wa ufaulu kwa kupata alama 'A' 32 na 'B+ '6 kati ya masomo 38 ya shahada ya Takwimu Bima (Actuarial Sc… Read More
MAAJABU:Uganda wazindua gari lisilotumia petrol. Uganda imezindua gari maalum la kipekee katika kanda ya Afrika mashariki maarufu kama hybrid electric car.Uzinduzi wa gari hilo ulifanyika katika mji mkuu wa Kenya Nairobi. Lakini je, hybrid electric car ni gari la ai… Read More
Baada ya kuhaha kwa takribani miaka miaka kumi,wanasayansi wafanikiwa kupeleka kifaa kwenye kimondoWanasanyansi wa safari za anga za mbali wamejawa na shauku ya kutaka thibitisho kwamba Chombo kilichopelekwa na kutua kwenye kimondo au nyota mkia yaani Comet iliyo umbali wa zaidi ya kilometa nusu bilioni kutoka duniani. Hap… Read More
Guiness wawakutanisha mwanaume mfupi na mrefu duniani Ijumaa ya jana (November 14) mwanaume mrefu kuliko wote duniani na mfupi kuliko wote walikutana katika tukio lililofanyika London ambapo walipiga picha ya pamoja wakipeana mikono. Tukio h… Read More
0 comments:
Post a Comment