Facebook

Tuesday 23 September 2014

Kiumbe cha ajabu kutoka baharini chaonekana Pemba.

Taarifa zilizotufikia BantuTz hivi punde kutoka huko Pemba ni kwamba;

Wananchi wa Kengeja Likoni,Kisiwani Pemba wameshuhudia kiumbe kikubwa na cha ajabu kilichotoka Baharini na kuja hadi nchi kavu kikiwa kinaelea baada ya kufariki.

Watu wengi wa Kengeja ambao wanajishughulisha na uvuvi wanasema kwamba kiumbe hicho ni Nyangumi huku wengine wanasadiki kusema kwamba ni Chongowe na baadhi wanasema hawajui ni aina gani ya Kiumbe.

Vijana wa tawi la Likoni zaidi ya 200 wamejitokeza katika fukwe za bahari hiyo kukishangaa kiumbe hicho cha ajabu chenye urefu wa Mita 40,Upana wa Mita 25 na amekwenda juu zaidi ya Mita 15.

Hakika ni kiumbe cha ajabu;Endelea kutembelea www.bantutz.com uweze kujua kila kitakachokuwa kinajiri huko Kengeja Likoni,Kisiwani Pemba kuhusiana na kiumbe hicho cha ajabu.

Credited by-Oscar Kiria.

0 comments:

Post a Comment