Wafungwa wawili wamepigwa risasi
walipokuwa wakijaribu kutoroka kutoka
katika mahakama moja nchini Afrika
Kusini.
Afisa mmoja kutoka wizara ya sheria aliambia
chama cha wanahabari nchini humo kwamba
wafungwa waliokuwa wanasubiri kusikilizwa
kwa kesi yao waliokota silaha kutoka kwenye
jaa la taka.
Inaarifiwa wafungwa hao walianza kufyatuliana
risasi na maafisa wa polisi.
Tukio hilo lilitokea katika mahakama kuu mtaa
wa Mthatha katika mkoa wa Eastern Cape.
Mthunzi Mhaga, ambaye ni waziri wa sheria,
alisema kuwa mfungwa mmoja alijeruhiwa
mguuni wakati wa ufyatulianaji risasi.
''Walijaribu kutoroka walipoingia ndani ya
majengo ya mahakama , '' alisema bwana
Mhaga.
''Baada ya kuipata bunduki, walianza
kufyatuliana risasi na maafisa wa polisi, ''
aliongeza kusema bwana Mhaga.
Alisema kuwa polisi waliweza kudhibiti hali.
Kufuatia visa vya hivi karibuni vya ufyatulianaji
risasi mahakamani mjini Pretoria na Cape
Town, waziri wa sheria alisema kuwa
atahakikisha uwepo wa sheria z akudhibiti
ulinzi katika majengo ya mahakama.
Wednesday, 10 September 2014
Wafungwa wapigwa risasi mahakamani Afrika Kusini.
Related Posts:
Polisi wazuia milango ya Bunge,Wabunge waruka ukuta kuingia ndani,mabomu ya yatumika kuwatuliza. Spika wa Bunge la Nchi ya Nigeria,Aminu Tambuwal amelazimika kuingia ndani ya Bunge kupitia mlango mdogo wa dharura baada ya Polisi kufunga milango ya Bunge hilo kwa sababu za kiusalama. Spika huyo alijitambulisha kwa… Read More
WANAWAKE WALIPWA KWA KUWANYONYESHA WATOTO UINGEREZA.Matokeo ya awali ya mpango wa kulipa wanawake ili kuwashawishi kunyonyesha watoto umeonesha matokeo mazuri, watafiti wameeleza. Wakina mama katika maeneo matatu ya Derbyshire,South Yorkshire nchini Uingereza ambapo kiwango ch… Read More
Kifo cha Mtoto mchanga chazua tafrani Uganda. Shughuli za mazishi ya mtoto wa miaka miwili zimefanyika nchini Uganda, mtoto ambaye kifo chake kimezua ghadhabu baada ya mtoto huyo kugongwa na gari la halmashauri ya jiji la Kampala ,baada ya mama yake kukamatwa akiu… Read More
BantuTz MAGAZETINI-Soma kilichoandikwa katika Magazeti ya leo Novemba 22 BantuTz MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusoma na kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma kupata … Read More
Yule rais wa kwanza Mzungu Afrika,atimuliwa na Chama chake.Chama tawala nchini Zambia (PF) kimemtimua kaimu rais wa nchi hiyo Guys Scott kutoka chamani na kuvunja utaratibu wa katiba. Taarifa hii ni kwa mujibu wa msemaji wa chama hicho. ''Amekuwa akiwaajiri na kuwafuta watu kazi ovyo… Read More
0 comments:
Post a Comment