Facebook

Thursday 25 September 2014

Magaidi wa Algeria wamchinja mtalii kutoka Ufaransa kuiunga mkono ISIS

Kundi la kigaidi la Jund al-Khilifa limemuua kwa
kumchinja mtalii wa Ufaransa ikiwa ni sehemu
ya ahadi yao kwa nchi hiyo ikiwa haitasitisha
mashambulizi dhidi ya kundi la ISIS nchini
Iraq.

Jumapili iliyopita, kundi hilo liliweka YouTube
video inayoonesha wapiganaji walijifunga
kitambaa usoni wakimfanyia tukio hilo mtalii
aliyetajwa kwa jina la Herve Gourdel mwenye
umri wa miaka 55, waliyemteka alipokuwa
nchini humo.

Ufaransa imeungana na Marekani katika
kampeni ya kushambulia kundi la ISIS lililoteka
sehemu kubwa nchini Iraq na Syria.

0 comments:

Post a Comment