Bwana mmoja jijini Mumbai nchini India,
amepewa talaka yake, baada ya kulalamika
kuwa hawezi kukata "kiu kubwa" aliyokuwa
nayo mke wake ya kufanya tendo la ndoa.
kwa mujibu wa tovuti ya Metro - Mwanaume
huyo akiwa amechoka, alifika katika
mahakama inayoshughulikia masuala ya
kifamilia mwezi Januari, akidai kuwa mke
wake amekuwa akimnyanyasa kwa kutaka
kufanya tendo la ndoa, tangu walipofunga
ndoa mwaka 2012, na kuwa amekuwa
akitumia 'mabavu na udikteta' wakati akitaka
jambo lake.
Na hakuishia hapo: bwana huyo ameiambia
mahakama kuwa mke wake pia alithubutu
hata kumpa dawa za kuongeza nguvu, na
kutishia 'kutembea' na wanaume wengine
kama atashindwa kukata kiu yake kubwa.
Mume huyo akiwa taabani- ambaye amesema
amesumbuliwa na maradhi ya kidole tumbo
'appendicitis' kutokana na kutopumzika,
alipewa talaka aliyokuwa akidai.
"Kwa kuwa mshtakiwa (mke) hakutokea
mahakamani, ushahidi wa mshtaki (mume)
haujapingwa. Na hivyo mahakama hii haina
budi, ila kukubali ushahidi uliowasilisha"
amesema Jaji Laxmi Rao.
Monday, 8 September 2014
MUME ADAI TALAKA BAADA YA KUSHINDWA "MAJUKUMU YA NDOA"
Related Posts:
BantuTz MAGAZINE-Soma kilichoandikwa katika Magazeti ya Tanzania leo Novemba 18 BantuTz MAGAZETINI-Ni uratatibu ambao BantuTz imeuanzisha ili kuwawezesha wadau wote wa Bantu waweze kusoma na kupitia kurasa za magazeti mbalimbali nchini kila siku asubuhi ili kuwasogezea karibu zaidi huduma ku… Read More
Je,wajua kuna waombolezaji wa kulipwa ? Kila Alhamisi na Ijumaa, shughuli katika mji wa Kisumu, magharibi mwa Kenya, huvurugika kwa sababu mamia ya waendesha pikipiki huzuia barabara kutokana na kukodiwa kuomboleza msiba kwa malipo. Kelele za saut… Read More
Mwizi akamatwa akiwa ameficha nyama sehemu za siri-Dar es SalaamUkistajaabu ya Musa utayaona ya Firauni. Hivi punde BantuTz tumepokea taarifa kutoka kwa ripota wetu aliye maeneo ya Magomeni kwamba kuna mwizi amekatawa katika 'Pub' moja maarufu sana maeneo hayo kwa uchomaji wa nyama ya Ngu… Read More
Maajabu ya mapacha wanaoshirikiana kila kitu hadi Mpenzi. Huwa si kitu cha ajabu kuona mapacha wakifanana kila kitu ndani ya familia hadi kusababisha watu kuwachanganya pindi wanapokutana nao kama hawajawazoea kuwaona kila siku. Mara nyingi mapacha wamekua wakishirikiana kat… Read More
Bwana harusi ampa talala Bibi harusi siku ya Kufunga Ndoa.Bwana harusi mmoja kutoka Saudi Arabia amempa talaka mkewe siku ya harusi baada ya kumuona uso wake kwa mara ya kwanza wakati mpiga picha alipotaka kuwapiga picha. Maharusi hao kutoka mji wa magharibi wa Saudia,Medinah waliku… Read More
0 comments:
Post a Comment