Facebook

Monday, 8 September 2014

MAJESHI YATUHUMIWA KUBAKA SOMALIA

Shirika la kutetea haki za binaadam la Human
Rights Watch, limetuhumu majeshi ya Umoja wa
Afrika yaliyopo Somalia kwa kubaka wanawake
na wasichana, na pia kudai ngono ili kuwapa
chakua cha misaada. Taarifa iliyoandikwa
kutokana na ushuhuda uliotolewa na wanawake
na wasichana ishirini na mmoja, imesema baadhi
ya wanajeshi kutoka Burundi na Uganda
walitumia ahadi ya kuwapa misaada ya
kibinaadam ili kuwashawishi wanawake na
wasichana kufanya nao tendo la ndoa. Human
Rights Watch imesema wanawake walinyanyaswa
kijinsia wakati wakitafuta huduma za afya au
maji katika kambi za Umoja wa Afrika. AU
imesema itachunguza tuhuma hizo. Wanajeshi
wapatao elfu ishirini na mbili kutoka mataifa
kadhaa yamekuwa yakipambana na al-Shabaab
nchini Somalia kwa miaka saba iliyopita.

Related Posts:

  • " Game of Thrones" yajinyakulia tuzo kubwa Marekani. Tamasha kubwa la kila mwaka Emmys Awards, la kutoa tuzo kwa vipindi vya televisheni limefanyika mjini Los Angeles Marekani. Kipindi cha Game of Thrones, kimenyakua matuzo mengi zaidi ikiwemo makala bora zaidi. Viola Davis nay… Read More
  • Wanasayansi watengeneza figo maabara. Je una matatizo ya figo ? Ikiwa jibu lako ni ndiyo kuwa na subira, maanake hivi karibuni figo zilizoundwa kwenye viwanda na maabara vitakuwepo kuwasaidia. Nafahamu kuwa waganga wengi wamewaahidi tiba lakini hii sio hekaya tu… Read More
  • Panya wasababisha kifo 'Jela ya Mandela'Watu karibu 4,000 wameondolewa kutoka jela ya Pollsmoor nchini Afrika Kusini baada ya panya wengi kuvamia gereza hilo na kusababisha kifo cha mfungwa mmoja. Kiongozi wa zamani wa nchi hiyo Nelson Mandela aliwahi kufungwa kati… Read More
  • Papa awasili Marekani apokewa na ObamaKiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amewasili nchini Marekani katika siku ya kwanza ya ziara ya kihistoria nchini humo ambapo amelakiwa na Rais wa nchi hiyo Barack Obama. Papa Francis aliwasili kwenye uwanja wa n… Read More
  • Bomu laua watu 6 katika makao ya Rais Somalia.Bomu lililotegwa ndani ya gari limelipuka karibu na lango kuu la jumba la rais katika mji mkuu wa Mogadishu. Takriban watu sita wamefariki,ikiwemo walinzi wa rais.Raia mmoja wa Uturuki pia aliuawa. Wengine 10 waliripotiwa kuj… Read More

0 comments:

Post a Comment