Jaji anayetoa uamuzi katika kesi ya mauaji
inayomkabili Oscar Pistorius, amesema
upande wa mashitaka umekosa
kuthibitishia kikamilifu shitaka kuu la
kwanza dhidi ya Pistorius kuwa alikusudia
kumuua mpenzi wake Reeva Steenkamp.
Hata hivyo jaji huyo Thokozile Masipa
amepinga ushahidi wa upande wa utetezi
kwamba mwanariadha huyo hakunuia kutenda
uhalifu alipomuua mpenzi wake Reeva.
Pistorius alikiri kumuua mpenzi wake Reeva
Steenkamp nyumbani kwake mwaka jana lakini
amekana kumuua kwa maksudi , akisema
alidhani kuwa mwizi alikuwa amevamia
nyumba yake.
Upande wa mshitaka unasisitiza kuwa Pistorius
alimuua Reeva kwa maksudi,baada ya wapenzi
hao wawili kutofautiana.
Mandishi mmoja anasema kuwa jaji Thokozile
Masipa heunda akachukua hadi Ijumaa
kumaliza uamuzi wake.
Pia atakuwa anaangalia kwa makini ukweli wa
mashahidi waliotoa ushaidi wao katika kesi
hiyo akiwemo Pistorius mwenyewe.
Pistorius huenda akafungwa jela miaka 25 ikiwa
atapatikana na hatia ya kumuua mpenzi wake.
Oscar Pestorius amekana mashitaka ya kumuua
mpenzi wake Reeva Steenkamp katika siku ya
wapendanao ya Valentine mwaka jana.
Mwendesha mashitaka anasisitiza kuwa
Pestorius alimpiga risasi aliyekuwa mpenziwe
Reeva baaya ya ugomvi baina yao lakini
amejitetea akisema alimpiga risasi kimakosa
akidhani mwizi amevamia nyumba yake.
Friday, 12 September 2014
Mahakama:Pistorius hakukusudia kuua
Related Posts:
Wanasayansi watengeneza figo maabara. Je una matatizo ya figo ? Ikiwa jibu lako ni ndiyo kuwa na subira, maanake hivi karibuni figo zilizoundwa kwenye viwanda na maabara vitakuwepo kuwasaidia. Nafahamu kuwa waganga wengi wamewaahidi tiba lakini hii sio hekaya tu… Read More
Viongozi wa Upinzani wavalia sare za wanafunzi KenyaBaadhi ya viongozi wa upinzani nchini Kenya wamevalia mavazi yanayofanana na sare za wanafunzi wakiitaka serikali kulipa walimu nyongeza ya mishahara. Walimu wamekuwa mgomoni tangu kufunguliwa kwa muhula wa tatu na Serikali i… Read More
Akamatwa kwa kuhifadhi sehemu za siriMaafisa wa polisi nchini Afrika Kusini wameomba kupewahabari zaidi baada ya kumkamata raia mmoja wa Denmark kwa madai ya kuhifadhi sehemu za siri za wanawake 21 katika jokovu. Peter Fredekrisen,ambaye anamiliki maduka mawili … Read More
Papa awasili Marekani apokewa na ObamaKiongozi wa Kanisa Katoliki duniani Papa Francis amewasili nchini Marekani katika siku ya kwanza ya ziara ya kihistoria nchini humo ambapo amelakiwa na Rais wa nchi hiyo Barack Obama. Papa Francis aliwasili kwenye uwanja wa n… Read More
Magari yalioibwa Uingereza yapatikana UgandaWapelelezi waliokuwa wakilitafuta gari moja aina la Lexus lililoibwa mjini London nchini Uingereza wamelipata nchini Uganda. Gari hilo lilikuwa na kifaa kinachoonyesha liliko. Walipolipata nchini Uganda ,lilikuwa miongoni mwa… Read More
0 comments:
Post a Comment