Facebook

Friday 26 September 2014

Mchinjaji wa kundi la Islamic State abainika.

Mkurugenzi mkuu wa FBI James Comey
amesema kitengo chake kimemtambua
mtu ambaye huficha sura yake ambaye ni
muuaji,ambaye pia huoneshwa wakati
akiwachinja mateka watatu kwenye video
inayo nadi wanamgambo wa dola ya kiislam
IS.

Pamoja na hayo Bwana Comey amegoma
kuutaja uraia wa mtu huyo ama hata kutaja
jina lake,ingawa imeshajulikana lafudhi ya mtu
huyo kuwa ni mwenye asili ya mji wa London,
na Comey amesema kwamba utambuzi wa mtu
huyo umefanikishwa kwa msaada mkubwa wa
marafiki wa kimataifa.

Muuaji huyo wa waandishi James Foley na
Steven Sotloff pamoja na mfanyakazi wa
kujitolea David Haines walipigwa picha ya
video na kuwekwa kwenye mitandao na
wanamgambo hao wa dola ya kiislam na
kusaidia kufanya maamuzi juu ya mipango ya
wapiganaji wa jihad.

Chanzo:BBC

0 comments:

Post a Comment