Gesi ya Chlorine ilitumika katika
kuwashambulia watu Kaskazini mwa Syria
mwaka huu, hii ni kwa mujibu wa shirika la
kimataifa ambalo linanuia kuweka sheria
zinazoharamisha silaha za kemikali.
Shirika hilo, (OPCW) linasema lina ushahidi
kuonyesha kuwa gesi ya Chlorine ilitumika
katika kuwashambulia wakazi .
Shambulizi lilifanyika mapema mwaka huu,
katika vijiji vilivyo karibu na maeneo ambako
waasi wamekuwa wakipigania na wanajeshi wa
serikali.
Shirika la OPCW limekuwa likijihusisha na
juhudi za kuharibu silaha za kemikali nchini
Syria.
Mwaka mmoja uliopita, Syria ilitangaza
kuharibu silaha za kemikali zilizokuwa
zimewekwa nchini humo kuambatana na sheria
za kimataifa.
Hata hivyo, Syria haikushurutishwa kutangaza
kiwango cha silaha ilizonazo, ambazo
zinaonekana kuwa za kemikali.
Ripoti hii ya hivi karibuni inasma kuwa
kemikali za sumu zilitumiwa kuwashambulia
watu vijijini hasa katika maeneo yaTalmanes, Al
Tamanah na Kafr Zeta Kaskazini ya Syria.
Kadhalika ripoti hiyo inasema kuwa inaamini
kwamba kemikali ya Chlorine ndiyo iliyotumika
katika kuwashambulia wanakijiji.
Inasema wanajua kwamba ni gesi ya Chlorine
iliyotumika kutokana na dalili walizokuwa nazo
wanakijiji , walivyokuwa baada ya matibabu
pamoja na maelezo kuhusu gesi hiyo.
Friday, 12 September 2014
Syria yashutumiwa kutumia Gesi ya Chlorine dhidi ya wakazi
By Unknown at Friday, September 12, 2014
No comments
Related Posts:
Alichopost Rihanna baada ya Ujeruman kushinda Kombe la Dunia Msanii wa R&B Rihanna ame-tweet picha hii akiwa na Bastian Schweinsteiger na Lucas Lukas Podolski baada ya Ujerumani kushinda Kombe la Dunia jana usiku.. … Read More
Tetesi za usajili katika magazeti mbalimbali barani Ulaya. TETESI ZA SOKA ULAYA Mshambuliaji wa Uholanzi na Bayern Munich Arjen Robben, 30, amekataa 'ofa' ya kujiunga na meneja wake Louis van Gaal, Old Trafford (Daily Telegraph), Meneja wa Arsenal, Arsene Wenge… Read More
Ujerumani bingwa wa kombe la dunia Ujerumani ndio mabingwa wa kombe la dunia Brazil 2014 Mario Götze anaipatia Ujerumani bao la ushindi. Ujerumani wanakuwa timu ya kwanza ya kutoka bara Ulaya kutwaa kombe la dunia katika mchuano ulioandaliwa Kusini mw… Read More
UFARANSA KUUNDA JESHI KUPAMBANA NA MAKUNDI YA JIHAD Ufaransa itaanzisha shughuli mpya za kijeshi katika eneo la Sahel, Afrika Kaskazini, katika juhudi za kuzuia kuibuka kwa makundi ya jihadi. Takriban wanajeshi 3,000 watapelekwa huko, kwa pamoja na wanajeshi kutoka… Read More
Messi na Nuer wajinyakulia tuzo. Messi akipokea tuzo la ''Golden Ball'' Lionel Messi, ambaye alipoteza fursa ya kutwaa kombe la dunia aliambulia tuzo la mchezaji bora katika mchuano hu… Read More
0 comments:
Post a Comment