Facebook

Wednesday 10 September 2014

FAIDA YA MAN UTD 'KUTETEREKA'

Manchester United imetangaza kuporomoka kwa
faida ya kila mwaka wa fedha katika mwaka
ambao David Moyes alikuwa meneja. Klabu hiyo
ya Ligi Kuu ya England imesema kipato halisi
kimeporomoka kwa asilimia 84 na kufikia
takriban dola milioni 45. Klabu hiyo imesema
inatarajia mapato yake ya mwaka 2015 kushuka
kutokana na klabu hiyo kushindwa kufuzu
kucheza Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya kwanza
tangu msimu wa mwaka 1994-95. Klabu hiyo
imesema Moyes na wasaidizi wake walilipwa zaidi
ya dola milioni 8 kama fidia kufuatia kufukuzwa
kazi mwezi Aprili, chini ya mwaka mmoja tangu
apewe kazi hiyo.

0 comments:

Post a Comment