Facebook

Thursday, 4 September 2014

Bibi aliyezaliwa mwaka 1887 ambaye sasa hivi ana mika 127 aeleza siri ya kuishi miaka mingi kiasi hicho.


Mwanamke wa Mexicana, Leandra Becerra mwenye umri wa miaka 127 anaetajwa kuwa mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani ameeleza siri ya kuishi miaka mingi zaidi.

Kwa mujibu wa mjukuu wake mwenye umri wa miaka 45, bibi huyo alimueleza kuwa siri ya ‘yeye’ kuishi miaka mingi ni kula vizuri, kulala kwa muda mrefu na kuishi bila kuolewa.

Bi Leandra ambaye alizaliwa August 31, 1887 alikuwa mpiganaji wakati wa mapinduzi ya Mexico mwaka 1910-1919 na alikuwa kiongozi wa kundi la ‘Adelitas’ ambalo lilikuwa linaundwa na wanawake wanaoenda vitani na waume zao.

Bibi huyo ambaye ana wajukuu wengi huku mjukuu wake mkubwa akiwa na umri wa miaka 73, tayari ameshawazika watoto wake watano.
Mjukuu wake aliiambia gazeti la El Hozizonte la Mexico kuwa bibi huyo hivi sasa anatatizo la kubwa la kusikia.

Ameeleza kuwa bibi huyo mara nyingine hulala mfululizo kwa muda wa siku tatu huku akipewa chakula pale anaposhituka.
Lakini akiamka hupenda kula mlo kamili kwa uhakika, kuimba, kutaniana na kusimulia hadithi mbalimbali zinazohusu maisha na mapambano ya mapinduzi ya Mexico.

Tofauti na wazee wengi, bi Leandra yeye hana tatizo la sukari hivyo anakula vitu vya sukari na chocolate kadri awezavyo.

Related Posts:

  • ANGALIA PICHA MWANAMAMA MWENYE MATUKIO YA AJABU  Kwa jina unaweza muita Leilani Franco(Backbend)  ana uraia wa nchi mbili (Uingereza / Philippines) alisafiri katika nafasi umbali wa 20m  katika muda wadk  10.05  katika  tamasha la Royal… Read More
  • Akimbiwa na Mkewe baada ya madaktari kuupunguza uume wake kwa bahati mbaya Madaktari nchini Canada wameingia katika matitizo makubwa baada ya kukosea na kumkata mwanaume mmoja sehemu ya uume wake na kupunguza kwa urefu wa inch 1 (sentimeta 2.5).Kwa mujibu wa QMI la Canada, mwanaume huyo anad… Read More
  • Je,wajua kuna waombolezaji wa kulipwa ?   Kila Alhamisi na Ijumaa, shughuli katika mji wa Kisumu, magharibi mwa Kenya, huvurugika kwa sababu mamia ya waendesha pikipiki huzuia barabara kutokana na kukodiwa kuomboleza msiba kwa malipo. Kelele za saut… Read More
  • Harusi ya Nyani yatia Fora India Zaidi ya wakazi 200 katika kijiji kimoja kaskazini mwa India wamehudhuria sherehe ya harusi ya nyani wawili. Harusi hiyo iliandaliwa na mmiliki wa nyani hao, ambaye alisema nyani dume ni kama "mwanaye". Sherehe hiyo ilif… Read More
  • MTOTO AMUOA MAMA YAKE WA KAMBO Bwana mmoja nchini Ufaransa amemuoa mke wa zamani wa baba yake (mama yake wa kambo) baada ya kushinda kesi iliyodumu kwa miezi kadhaa. Harusi ya Eric Holder, 45, na aliyekuwa mama yake wa kambo Elisabeth Lorentz, 48, i… Read More

0 comments:

Post a Comment