Facebook

Wednesday, 21 May 2014

Man City kununua wachezaji

Manchester City kununua licha ya faini ya UEFA
Mwenyekiti wa Manchester City Khaldoon Al Mubarak amesema kuwa mabingwa hao wapya wa ligi kuu ya Uingereza wataimarisha kikosi chao licha ya marufuku waliopigwa na shirikisho la kandanda barani ulaya UEFA kwa kukiuka kanuni za matumizi ya fedha.
City ilipigwa faini ya pauni milioni £49m, mbali na kuruhusiwa kuwasajili wachezaji 21 pekee katika msimu huu mpya kushiriki katika ligi kuu ya mabingwa barani ulaya.
Kanuni hiyo inamaanisha kuwa Mabingwa hao watatumia pauni milioni £49m kuwanunua wachezaji mbali na idadi yeyote itakayopatikana kutokana na mauzo ya wachezaji.
City kununua Wachezaji licha ya vikwazo vya UEFA
Manchester city walitwaa ubingwa wa ligi msimu huu baada ya kukamilisha msimu wakiwa na pointi mbili zaidi ya wapinzani wao wa karibu Liverpool.
Kutokana na faini hiyo ya Uefa Manchester City wameshurutishwa kutotumia mshahara unaozidi ule waliotumia msimu huu katika msimu ujao wa 2014-15 .
Licha ya hayo Mubarak, amesema kuwa wamiliki wa klabu hyo wanafahamu fika matakwa ya UEFA na kuwa watamuunga mkono kwa hali na mali kocha Manuel Pellegrini wakati wa usajili msimu ujao.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 60 kutoka Chile mwaka 2013 baada ya Roberto Mancini kufutwa kazi.

Related Posts:

  • Man United wapewa nafasi kubwa kumnasa Gundogan.Manchester United inamwinda mchezaji IIkay Gundogan kutoka Dortmund lakini taarifa zinasema mchezaji huyo yupo katika mazungumzo na vilabu vingine vya Bayern Munich na Barcelona. Timu za Arsenal, Chelsea zinatajwa kumchu… Read More
  • Walcott akataa kuzungumzia mkataba mpya ArsenalTheo Walcott hataki kuonyesha muelekeo wake ndani ya Arsenal ingawa mkataba wake umebakisha mwaka mmoja kuisha.Walcott alifunga katika fainali ya FA dhidi ya Aston Villa kwa ushindi wa 4 - 0.Mchezaji huyo ameviambia vyombo … Read More
  • Brendan Rodgers asalia Liverpool. Brendan Rodgers anabaki klabuni Liverpool baada ya mazungumzo mazuri na mwenyekiti wa timu hiyo Tom Werner. Mazungumzo hayo yame mbakisha Rodgers kuwa meneja wa Liverpool. Je! maamuzi ya kumbakisha Brendan Anfield, ikiwa t… Read More
  • Van Persie hatihati kusalia Man United Mshambuliaji wa Manchester United Robin van Persie amekubali kuondolewa Old Trafford baada ya kupitia magumu msimu huu.Mshambuliaji wa Manchester United ana mwaka mmoja tu wa kumaliza mkataba wake wa sasa.Van Persie ana ma… Read More
  • Schneiderlin kutua Man United kwa ada ya Euro milioni 25Manchester United imevutiwa na kutaka kumsaini mchezaji kiungo wa Southampton Morgan Schneiderlin..Kiungo huyo wa miaka 25 ni mmoja wa viungo waliocheza vizuri msimu uliomalizika wa Premier League.Timu ya Arsenal na Tottenha… Read More

0 comments:

Post a Comment