Facebook

Tuesday, 17 June 2014

Mourinho amuonya Roy Hodgson kuhusu Rooney

Kocha Jose Mourinho amekosoa nafasi aliyopangwa Wayne Rooney kwenye mechi ya England na Italia huko Manaus , Brazil. Italia walishinda 2-1.
Kocha Jose Mourinho amekosoa nafasi aliyopangwa Wayne Rooney kwenye mechi ya England na Italia huko Manaus, Brazil. Italia walishinda 2-1.
Jose Mourinho ameyavulia nguo maji yasiyo yake kwa kutoa tathmini ya matatizo ya England, Kombe la Dunia kwa kumuonya Roy Hodgson kuwa: “Wayne Rooney si hatari akichezeshwa pembeni”.
Rooney alitoa msaada mkubwa kwa Daniel Sturridge ambaye alifunga goli la kusawazisha huko Manaus ila uwezo wake wa pembeni ambao aliwekwa na kocha Roy Hodgson haukuweza kutoa msaada mkubwa kwa mshambuliaji pekee.
Na kocha wa Chelsea Mourinho, ambaye alijaribu kumsainisha Rooney msimu uliopita, alisema; “Sidhani kama ni nafasi nzuri kwa Rooney, ila mara nyingi wachezaji hawana budi kujitoa mhanga kwa ajili ya timu zao na nafikiri alifanya vizuri”.

Tumehamia katika site hii mpya na bado tuko katika maboresho,hii ni katika hatua za awali kabisa kuiboresha site yetu na utoaji wa habari na burudani.Vitu vingi vitaonekana katika site hii mpya hivi karibuni.Endelea kutembelea www.bantutz.com

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment